Skip to main content

Posts

Showing posts from December 1, 2014

MANISPAA YA IRINGA WAADHIMISHA SIKU YA UKIMWI DUNIANI KWA KUTOA MISAADA YA VYA KULA KWA YATIMA

Baadhi ya watoto yatima wa kituo cha Daru Fatma kinachomilikiwa na taasisi ya kiislamu Dhinureyn (Dhinureyn Islamic foundation) wakimsikiliza  naibu meya wa manispaa ya iringa Gervas Ndaki alipotembelea kituo hicho na kutoa msaada wa vyakula. Ndaki alikuwa kiongozi wa msafara wa timu ya manispaa ya iringa pamoja na baraza la madiwani walipotembea kituo hicho kama sehemu ya maadhimisho ua siku ya ukimwi duniani. Mkuu wa Idara ya Ustawi wa  Jamii katika taasisi ya kiislamu Dhinureyn (Dhinureyn Islamic foundation) Abbas Upete wakitoa shukrani kwa viongozi wa halmashauri ya manispaa  kwa msaada wa vyakula kwa niaba ya taasisi hiyo. Taasisi hiyo ya Dhinureyn inamiliki vituo viwili vya watoto yatima ambavyo ni Daru Fatma ambacho kina watoto yatima wasichana 51 na Daru Bilali kwa upande wa wavulana ambao wapo jumla 50. Naibu Meya wa Manispaa ya Iringa Gervas Ndaki ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Ilala akikabidhi msaada wa vyakula kwa watoto yatima wa kituo cha Hu...