Na Friday Simbaya, Iringa MKUU wa Mkoa wa Iringa Amina Masenza amepongeza Mradi wa NAFAKA kwa juhudi za kuinua uchumi wa vikundi vya wakulima na kuleta maendeleo katika sekta ya kilimo. Alisema kuwa Kilimo kinatoa mchango mkubwa wa ajira kwa vijana na wanawake walioko vijijini na mijini kwa maendeleo yetu na Taifa kwa ujumla. Masenza alisema hayo jana wakati wa kukabidhi zana za kilimo kwa wakulima katika vikundi vya uzalishaji, na kuongeza kuwa zana hizo za kilimo zitasaidia wakulima kuongeza tija, uzalisahji na kufanya shughuli za kilimo kwa wakati. Pia, alisema kuwa nyenzo hizo za kilimo zitawezesha vijana na wanawake kushiriki katika kilimo kwa mafanikio makubwa ikiwa pamoja na kukuza uchumi wa kipato katika ngazi ya kaya pamoja na kupunguza umasikini kwenye mkoa wa Iringa. “Serikali inahimiza sana wakulima wadogowadogo, wakulima wakati na wakubwa kutumia zana bora za kilimo katika shughuli za uzalishaji mazao ili kuongez...