Wanafunzi wa Shule ya Msingi ya Lupefu, Lugarawa wakiwa
darasani na Mwalimu Mary Mhagama huku wakiwa wamebanana saba kwenye dawati moja
lenye uwezo wa watoto watatu.
WANAFUNZI
katika Shule ya Msingi ya Lupefu iliyoko Kata ya Lugarawa wilayani Ludewa,
mkoani Iringa wako hatarini kukatika miguu na viungo vingine vya mwili kutokana
na kuliwa na funza mikono na miguu yao kunakosabishwa na uhaba wa madawati
ambapo sasa wanafunzi saba wanalazimika kukalia dawati moja.
Mwalimu
Mkuu wa shule hiyo Bi. Aprudensia Lugome amekiri kuwepo kwa matatizo hayo na
kuongeza kuwa hali hiyo inatokana na ukata wa fedha unaoikabili shule yake
pamoja na uelewa na mwamko mdogo wa wananchi juu ya elimu.
Lugome
alisema hulazimika kila wakati kununua pini madukani kwa fedha zake na kuwaita
wazazi wa wanafunzi wenye mafunza kufika shuleni kushiriki kuwatoa funza watoto
wao hata hivyo hufika wachache. ...
Pamlomo-Sauti Ya Jamii (SYJ) is essentially a digital news platform that shares different types of news updates — social, political, economic, sports, entertainment, and community stories. From the context you’ve given, it is based in Iringa, Tanzania, and functions mainly as an online outlet (likely through social media such as Facebook, YouTube, or other channels) where audiences can get real-time updates.