Na Friday Simbaya, Songea Mwenyekiti wa Kitongoji cha Mlimani katika Kijiji cha Peramiho ‘B’ wilayani Songea, mkoani Ruvuma, Bonventura Mhagama kwa kushirikiana na katibu wake, Asante Mbawa amesema mwananchi atakeyetukana matusi hadharani atatozwa faini ya shilingi elfu hamsini. Alisema kuwa kumezuka tabia kwa baadhi ya watu kitongojini kwa makusudi wameamua kutoa matusi ya nguoni hadharani kwa kisingizio cha kulewa pombe. Mwenyekiti huyo alisema hayo jana wakati wa mkutano wa kitongoji, ambapo alisisitiza kwamba ni wakati wa kutumia sheria ndogondogo kukomesha tabia ya watu kutukana matusi baada ya kutofautiana kauli. “Ni lazima tuishi katika jamii inayozingatia maadili, mtu mzima unapoporomosha matusi hadharani unamfundisha ni nini mtoto?” alihoji mwenyekiti huyo. Alisema kitendo hicho katika kitongoji hakitavumilika kwa sasa kwa sababu sheria ndogondogo zitatumika kumshitaki mtu yeyote atakayetukana mwenzake ili mradi kuwepo na ushahidi. Katika m...
Pamlomo-Sauti Ya Jamii (SYJ) is essentially a digital news platform that shares different types of news updates — social, political, economic, sports, entertainment, and community stories. From the context you’ve given, it is based in Iringa, Tanzania, and functions mainly as an online outlet (likely through social media such as Facebook, YouTube, or other channels) where audiences can get real-time updates.