Skip to main content

Posts

Showing posts from November 26, 2014

MRADI WA KUWAWEZESHA AKINA MAMA KATIKA KILIMO PAWAGA

Mwakilishi wa ubalozi wa marekani David Feldmann akihutubia mamia ya wakazi wa vijiji vya tarafa ya Pawaga wakati sherehe ya kufunga mafunzo ya mradi wa kuwawezesha akina katika kilimo kupitia asasi ya mpango salama wa maendeleo ya vijana (SYDS) kwa ufadhili ya watu wa marekani.  Alisema kuwa kilimo bora ni kile chenye kuleta tija na mafanikio. Jumla ya vikundi 43 vya wajasiliamali ambao ni sawasawa na wanawake na vijana zaidi ya 300   wa tarafa ya Pawaga wilayani Iringa, mkoa wa Iringa wamenufaika na mafunzo ya kuwezesha akina mama katika kilimo kutoka SYDS. Mafunzo hayo yaliendeshwa na asasi isiyo ya kiserikali ya mpango salama wa maendeleo ya vijana (SYDS) kwa ufadhili wa serikali ya marekani kupitia ubalozi wake nchini Tanzania. Akizungumza na waandishi wa habari wakati sherehe ya kufunga mradi huo wa mrejesho kwa vikundi, meneja mahusiano wa SYDS, Arnold Pangani alisema SYDS imejitoa   kuendeleza mapambano dhidi ya changamoto zinazowakabili we...