Skip to main content

Posts

Showing posts from August 2, 2015

MTOTO WA MAMA NTILIE JUMAA AWESO ASHINDA KWA KISHINDO UCHAGUZI WA NDANI CCM PANGANI

Ndugu Jumaa Aweso. Na Mohammed Hammie, Pangani, Tanga Mtoto wa mama ntilie mwenye uzao halisi kutoka wilayani Pangani mkoani Tanga, Ndugu Jumaa Aweso (pichani) ameibuka na ushindi wa kishindo katika uchaguzi wa ndani wa chama cha mapinduzi CCM. Akitangaza matokeo ya uchaguzi huo katibu wa CCM wilayani Pangani Bi Zaina Mlawa amesema kuwa, katika uchaguzi huo uliowashirikisha wagombea wapatao kumi na moja, Ndugu Aweso amekuwa wa kwanza miongoni mwa wagombea hao.

MWAKALEBELA, LUKUVI NA MGIMWA NDANI Y NYUMBA...!

MKUU wa wilaya ya Wanging’ombe, Frederick Mwakalebela ameibuka kidedea katika kura za maoni za kutafuta kuteuliwa kugombea ubunge jimbo la Iringa Mjini kwa kuwabwaga vibaya washindani wenzake 12. (Picha na Friday Simbaya) Iringa:   ZOEZI la kuhesabu kura za kuwania ubunge kwa tiketi ya chama cha  mapinduzi CCM Mkoa wa Iringa kwa majimbo matatu limeendelea vizuri. Jimbo la Iringa Mjini. Jimbo la Iringa mjini lilikuwa na wagombea 13 ambao ni Fredrick Mwakalebela ameshinda kwa kura 40388, Jesca Msambatavangu 2077, Yahaya  Msigwa 1097, Augustine Mahiga 745, Mahamood Madenge 423, Addo Mwasongwe  ,259, Nuru Hepautwa 191, Frank Kibiki 183, Maiko Mlowe 183, Fales Kibasa 171, Kiponda Stephen 135 Mwanilwa Joseph 79 na Adelino Gwilino 66.   Jumla  ya kura z zilikuwa 10,216 ,zilizoharibika 220 kura halali 9997. Jimbo la kalenga Wagombea ubunge Kwenye Jimbo la kalenga walikuwa watano ambao ni Abbas  Kandoro alipata kura 674, J...

DOSARI YAJITOKEZA KURA ZA MAONI UBUNGE JIMBO LA IRINGA MJINI, MGOMBEA ATAKA MCHAKATO USITISHWE

frank Kibiki ambaye pia ni Mwanahabari wa Magazeti ya Uhuru na Mzalendo wa mkoani  frank Kibiki akionyesha walivyo kosea jina lake.  na mwandishi wetu,iringa WAKATI  kura za maoni za kutafuta wagombea ubunge katika majimbo yote nchini kupitia  Chama cha Mapinduzi (CCM) zimekipigwa jana, mmoja kati ya wagombea 13 wanaotafuta  nafasi hiyo Jimbo la Iringa Mjini, Frank Kibiki anataka zoezi hilo jimboni humo  libatilishwe.