Skip to main content

Posts

Showing posts from April 27, 2015

WANAWAKE 512 WAGUNDULIKA NA KANSA YA SHINGO YA KIZAZI

MKOA wa Iringa umeweza kuchunguza kina mama 11,223 na kati hawa wanawake 512, (sawa na asilimia 4.6) waligundulika kuwa na mabadiliko ya awali na kupewa tiba katika kipindi cha kuanzia Januari 2014 mpaka Januari 2015. Hayo yalisemwa hivi karibuni na Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Uchumi, Mkoa wa Iringa, Adam Swai wakati wa mkutano wa kufunga na kutoa tathmini ya mradi wa kuhamasisha jamii kuhusu huduma za uchunguzi wa saratani ya mlango wa shingo ya kizazi.

Frank kibiki awaokoa watoto waliofanyiwa ukatili wa kijinsia mkoa wa Iringa

mwanahabari frank kibiki , aliyewahi kuwa katibu wa umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi (uvccm) ngazi ya wilaya kwa zaidi ya miaka 10 na ambaye ni mjumbe wa nec akiwa na watoto waliofanyiwa ukaliti wa kijisia pamoja mkuu wa kituo cha matumaini centre mwandishi wa habari wa gazeti la mzalendo na uhuru TUMAINI MSOWOYA KIBIKI akiwa na watoto waliofanyiwa ukatili wa kijinsia mwandishi wa habari wa gazeti la mzalendo na uhuru TUMAINI MSOWOYA KIBIKI akiwa na watoto waliofanyiwa ukatili wa kijinsia pamoja na mkuu wa kituo cha matumaini centre. na fredy mgunda,iringa Ukatili wa kijinsia kwa watoto wa kike ndio inaonekana kuwa sababu ya mkoa wa iringa kuzalisha wafanyakazi wengi wa kazi za ndani

UZINDUZI WA SHAMRA SHAMRA ZA MIAKA 70 YA UMOJA WA MATAIFA WAFANA JIJINI DAR

Cake maalum iliyoandaliwa kwenye sherehe za uzinduzi wa shamra shamra za miaka 70 ya Umoja wa Mataifa uliofanyika mwishoni mwa juma kwenye hoteli ya White Sands jijini Dar es Salaam. Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez (katikati) akiteta jambo na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la UN Women nchini Tanzania, Anna Collins kabla ya zoezi la kuwasha mishuma 70 kwenye cake hiyo ikiwa ni uzinduzi wa shamra shamra za miaka 70 ya Umoja wa Mataifa. Kushoto ni Mshehereshaji wa sherehe hizo Afisa Habari wa kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Usia Nkhoma Ledama. Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez (wa pili kulia) na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la UN Women nchini Tanzania, Anna Collins wakiwa wamejumuika na wafanyakazi wa mashirik...