Skip to main content

Posts

Showing posts from June 27, 2016

LEAT IMEANZA MCHAKATO WA KUZIWEZESHA SERIKALI ZA VIJIJI KUANDAA SHERIA NDOGO ZA USIMAMIZI WA MALIASILI NA MAZINGIRA

Katika kufikia malengo ya mradi wa ‘Ushiriki wa Wananchi katika Usimamizi wa Maliasili, unaotekelezwa mkoani Iringa; Timu ya Wanasheria Watetezi wa Mazingira kwa Vitendo (LEAT) imeanza mchakato wa kuziwezesha serikali za vijiji kuandaa sheria ndogo zitakazo waongoza katika usimamizi wa maliasili na mazingira.  Sheria hizo zitasaidia kupunguza uharibifu wa rasilimali misitu na wanyamapori ambazo zipo katika hatari ya kutoweka kutokana na uvunaji haramu.  Kabla ya kuanza utekelezaji wa mradi katika wilaya za Iringa na Mufindi, mkoani Iringa; LEAT ilifanya utafiti juu ya kiwango cha ushiriki wa wananchi katika usimamizi wa maliasili, pamoja na mambo mengine katika utafiti huo LEAT ilibaini kuwa baadhi ya vijiji havikuwa na sheria ndogo ambazo zingetumika kusimamia maliasili na mazingira. Kutokana na hali hiyo LEAT imeanza mchakato wa kuziwezesha serikali za vijiji kuandaa sheria hizo. Vijiji vitakavyo wezeshwa katika awamu ya kwanza ni vijiji vya Mbweleli, Kinyika...

SHEIKH JALALA AWAKUTANISHA MASHEIKH, MAIMAMU WA MADHEHEBU TOFAUTI, WAJADILI DHULMA DHIDI YA WAPALESTINA

Kiongozi Mkuu wa Waislam dhehebu la Shia Ithnasheriya Tanzania Sheikh Hemed Jalala akifafanua jambo kwa waandishi wa habari kuhusu siku ya Quds inayokumbukwa na Waislamu wote Duniani kote.Matembezi ya siku hiyo hapa nchini yanatarajiwa kuwa Tarehe mosi mwezi ujao. Masheikh na Maimamu wakiwa katika semina maalum inayohusu kutafakari juu ya kadhia ya Palestina, semina hiyo ilifanyika katika Msikiti wa Al Qadir Kigogo Post Daresalaam. Kiongozi Mkuu wa Waislam dhehebu la Shia Ithnasheriya Tanzania Sheikh Hemed Jalala amesema kila mwanadamu anawajibu kupiga vita dhidi ya matendo ya dhulma wanayofanyiwa Wapalestina. Hayo ameyasema jana katika semina maalum ya Quds, iliyowakutanisha Viongozi wa Dini, mbalimbali wakiwamo Maimam, Masheikh na Maustadhi kutoka Madhehebu mbalimbali ya Kiislam, semina iliyofanyika Masjid Ghadir, Kigogo Post Dar es salaam. Katika semina hiyo ya siku moja iliyokuwa na dhamira ya kujadili umuhimu wa kadhia ya Palestina na jinsi inav...

Tanzanians are being sentenced to jail for insulting their president on social media

Not all jokes get President Magufuli (right) laughing. (Reuters/Emmanuel Herman) WRITTEN BY Yomi Kazeem Making jokes about president John Magufuli can come at high personal cost in Tanzania. Yesterday, June 21, a local man Leonard Mulokozi was charged with the crime of insulting the president on Whatsapp, following a similar case earlier this month. Mulokozi’s message is alleged to have read: “Does this mean Magufuli doesn’t have advisors? Is he unadvisable? Or is he just a fool? He’s foolish, this fellow. He doesn’t consider the applicable laws before opening his mouth. Or does he suffer from an illness like that of [member of parliament] Mnyika?” Under a much-criticized cybercrime law passed last year, publishing information with the “intent to defame, threaten, abuse, insult, cause public panic, or encourage criminal offense” can now be classed as a crime . If found guilty, Mulokozi faces a similar sentence to Isaac Ababuki, who was found to have i...