Skip to main content

Posts

Showing posts from September 9, 2016

SAFARI ZA TUISHENI ZILIVYOMGEUZA MWALIMUU KUWA MZAZI MWENZIWE

Haya ni maneno ya Jackline Masisa (17), aliyekatiza masomo akiwa kidato cha kwanza katika shule ya sekondari Mondo wilayani Kishapu, baada ya kupewa mimba na mwalimu wa shule jirani na mahali alikokuwa anapata huduma ya masomo ya ziada au tuisheni. “Akimaliza kunifundisha, alikuwa ananishikashika na kunivua nguo, kisha kunilaza…” anaendelea kusimulia Jackline, akimueleza mwalimu huyo mwenye umri wa miaka 30 (jina linahifadhiwa). Anasema mwalimu huyo alimshawishi kuingia katika masomo ya ziada, yaani tuisheni, lakini baada ya muda wakageukia mapenzi.  Jackline anakiri alizamishwa katika mapenzi na mwalimu wake kwa ushawishi wa ‘posho’ ya Sh. 5000 na matokeo yake, hivi sasa ana mtoto mwenye miaka miwili analelewa na wazazi wake, baada ya mwalimu aliyempa mimba kumkana. Ilikuwaje baada ya wazazi kugundua yu mja mzito? Kwanza anaanza kusema namna alivyoingia katika maisha mapya ya ujauzito. Bila ya kujitambua ana hali gani wakati huo , Jackline anasimulia, huk...

MBUNGE COSATO CHUMI AANZA KUTATUA TATIZO LA MAJI

Bw Donsun Lee ambaye ni Mkurugenzi wa NGO ya Kutoka Korea ya Serving Friends International akikagua pump kwenye moja ya kisima kwenye shule ya Msingi Makalala, anayetizama ni Mbunge wa Mafinga Mjini Cosato Chumi Bw Donsun Lee ambaye ni Mkurugenzi wa NGO ya Kutoka Korea ya Serving Friends International akimsikiliza kwa makini Mhandisi wa Maji wa Mji wa Mafinga Eng Eradius.  Pichani baadhi ya wanafunzi na waalimu wa shule ya Msingi Makalala wakiwa katika picha ya pamoja na Mrs Lee na Mbunge wa Mafinga Mjini Cosato Chumi na fredy mgunda,iringa MBUNGE wa jimbo Mafinga mjini Cosato Chumi ameendeleza juhudi zake za kuwatafutia maendeleo wananchi wa jimbo lake kwa kufanya kazi kwa ukaribu na taasisi za kiserikali na zisizo za kiserikali za nje ya nchi ya Tanzania pamoja na taasisi za ndani. Hivi karibu balozi wa korea nchini Tanzania Bw Song Geum Young akiwa na NGO ya Kutoka Korea ya World share alitembelea jimbo la mafinga mjini kwa leng...