Skip to main content

Posts

Showing posts from August 24, 2016

KUUAWA KWA POLISI BENKI YA CRDB MBANDE JIJINI DAR ES SALAAM JESHI LA POLISI LAHUSISHA NA UKUTA

Kamishna Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi nchini, Nsato Marijan Mssanzya (CP), akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo kuhusu tukio la mauaji ya askari wanne katika Benki ya CRDB Tawi la Mbande yaliyotokea usiku wa kuamkia leo. Waandishi wa habari wakichukua taarifa hiyo. Wapiga picha na waandishi wakiwa bize kupata taarifa hiyo. Na Dotto Mwaibale KUFUATIA mauaji ya askari wanne yaliyotokea Kata ya Mbande Temeke kwa watu wanaodhaniwa ni majambazi kuvamia benki ya CRDB na kuwaua askari hao kwa kutumia silaha za moto jeshi la Polisi limetangaza kiama na kuwataka wahusika wote kujisalimisha. Katika hatua nyingine jeshi la polisi limehusisha tukio hilo na Umoja wa Kupinga Udikteta Tanzania (UKUTA) kufuatia matamko ya baadhi ya viongozi wa kisiasa ambao wamesikika katika majukwaa ya kisiasa wakihamasisha wafuasi wao wawashambulie askari wa Jeshi la Polisi. Kauli hiyo imetolewa na Kamishna Operesheni na Mafunzo wa ...

MCHUNGAJI RAPHAEL MWASIFIGA: HAIKUWA KAZI RAHISHI KUMJUA MUNGU

KANISA LA BAPTIST SINDE   Na Friday Simbaya, Mbeya “Nilizaliwa katika familia ya kipagani ambapo baba yangu mzazi alikuwa ni msaidizi wa chifu ambao waliitwa ‘Ifumu’, habari za dini na elimu kwake zilikuwa ni mwiko…” Hayo yalikuwa ni maneno ya Mchungaji Raphael Mwasifiga wa Kanisa la Baptist la Kanani, Makunguru Sinde, Mwanjelwa mkoani Mbeya. Mchungaji Mwasifiga alizaliwa mwaka 1953 katika kijiji cha Lukule Kiwira akiwa ni mtoto wa saba na wa mwisho katika familia ya Mzee Mwasifiga. Alisema kuwa alipenda sana kusoma shule na kujifunza dini lakini haikuwa kazi rahisi kutokana na baba yake kuona vitu kama hivyo ni vya kihuni. “Wakati ni kiwa mtoto nimechunga sana ng’ombe kijijini kwetu na baadaye niliamua kwenda shule na nilisoma mpaka darasa la saba mwaka 1968,” alisema Mch. Mwasifiga. Alisema kuwa baada ya kumaliza elimu ya msingi alikwenda kuishi na dada yake mjini Mbeya ndipo alipoanza kujishughulisha na masuala ya dini na baad...

KOREA KUSINI YATOA BILIONI NNE KUJENGA KITUO CHA TAARIFA KATIKA HIFADHI YA TAIFA YA SERENGETI

Wajumbe wa Kamati ya Maendeleo kwa Afrika katika Bnge la Korea Kusini wakiwasili katika uwanja mdogo wa ndege uliopo katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.  Meneja Masoko wa Shirika la Hifadhi za Taifa,TANAPA,Victor Ketance akipokea ugeni wa wajumbe kutoka Bunge la Korea Kusini walipotembelea Hifadhi ya Taifa ya Serengeti kwa ajili ya kutizama eneo la uwekezaji wa kituo cha kisasa cha taarifa za hifadhi hiyo. Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti (SENAPA) William Mwakilema akipokea ugeni wa wajumbe kutoka Bunge la Korea Kusini walipotembelea Hifadhi ya Taifa ya Serengeti kwa ajili ya kutizama eneo la uwekezaji wa kituo cha kisasa cha taarifa za hifadhi hiyo.  Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti (SENAPA) William Mwakilema akisalimiana na wadau wa utalii,Zainabu Ansel ,Mkurugenzi wa kampuni ya Utalii ya Zara(katikati) na Mkurugenzi wa Kibo Safari's Willy Chamburo.(kushoto) waliokuwepo uwanjani hapo.  Mkurugenzi wa Kampuni ya Kibo Safari's ,Wi...

DC STAKI ATENGA SIKU YA JUMATATU KUSHIRIKI SHUGHULI ZA MAENDELEO

Mkuu wa Wilaya ya Same Mkoani Kilimanjaro Mhe Rosemary Staki Senyamule akishiriki shughuli za maendeleo kwa kufyeka baadhi ya vichaka Mkuu wa Wilaya ya Same Mkoani Kilimanjaro Mhe Rosemary Staki Senyamule akizungumza na viongozi wa Kijiji na Kata ya Gonja Maore na baadhi ya wajumbe wa kamati ya siasa Wilaya Dc Senyamule akishiriki zoezi la kupanga matofali yaliyofyatuliwa na wananchi wenyewe kwa ajili ya miradi ya maendeleo Wilayani humo. Na Mathias Canal, Kilimanjaro Mkuu wa Wilaya ya Same Mkoani Kilimanjaro Mhe Rosemary Staki Senyamule ametenga Siku moja katika Juma ili kushiriki shughuli za maendeleo kwa kushirikiana na wananchi. Huu ni utaratibu ambao Mkuu huyo wa Wilaya ameuanzisha kwa muktadha wa kuchochea ari katika utendaji Kazi na uwajibikani kwa kila mwananchi ili kuimarisha na kusukuma kwa vitendo juhudi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Joseph Pombe Magufuli kwa vitendo na utekelezaji wa utendaj...

WANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI SINDE JIJINI MBEYA WAPO HATARINI KUUGUA MAGONJWA YA MLIPIKO

Wanafunzi wa Shule ya Msingi Sinde Kata ya Sinde katika Halmashauri ya Jiji la Mbeya, mkoani Mbeya wa kunywa maji kwenye chemchem ya maji wakati wa mapumziko jana. Wanafunzi hao wako hatarini kuugua magonjwa ya mlipuko kutokana na kunywa maji yasio safi na salama kutoka kwenye Korongo la maji lililopo karibu na shule hao kama ilivyokutwa na mpigapicha wetu. Korongo hilo maarufu kwa jina la Afrika linatumiwa pia na wakazi wa eneo hilo kwa ajili ya matumizi mbalimbali ya majumbani. Wanafunzi hao waliambia mpigapicha wa gazeti hili kuwa wapo baadhi ya wenzao ambao wameugua ugonjwa wa Kichocho pamoja na homa ya matumbo kutokana na kunywa maji hayo. Shule ya Msingi Sinde pia inakabiliwa na ukosefu maji ya bomba pamoja na ubovu wa miuudombinu ya vyoo vya wanafunzi. (Picha na Friday Simbaya)