Skip to main content

Posts

Showing posts from December 9, 2015

KIPINDI CHA 'TUWALINDE WATOTO WETU' KURUKA TENA ALHAMISI HII, CLOUDS TV

Mmiliki na mwendeshaji wa kipindi cha Tuwalinde Watoto Wetu, Janet Mwenda. Na Rabi Hume, Modewjiblog Kipindi cha Tuwalinde Watoto Wetu kilichokuwa kikirushwa na Clouds TV, Alhamisi ya wiki hii kinatarajiwa kuanza tena kuonekana kupitia Clouds TV Alhamisi ya Disemba 10, saa tatu kamili usiku. Akizungumza na Dewjiblog , Mmiliki na mwendeshaji wa kipindi hicho, Janet Mwenda amesema kuwa kipindi cha Alhamisi hii kinatarajiwa kuja na kitu kipya tofauti na vile walivyokizoea kuonekana hapo awali na hivyo kuwataka watazamaji kukaa tayari kuona kipindi bora kuhusu watoto na changamoto wanazokutana nazo. Amesema lengo la kipindi hicho ni kuwakumbusha wazazi na walezi majukumu yao kwa watoto wao na hatari wanazoweza kukutana nazo pindi wasiposimamiwa vizuri na watu wanaoishi nao na kupitia kipindi hicho wanaweza kuona maisha wanayokutana nayo watoto hao pindi wanapokuwa nje ya familia zinazowalea. “Kuna mambo jamii inakuwa haiyaamini kama yanatokea na tunachofanya ni ku...

MeTL GROUP YASHEREKEA SIKU YA UHURU KWA KUFANYA USAFI COCO BEACH

Na Rabi Hume, Modewjiblog Kampuni ya Mohamed Enterprises Tanzania Limited (MeTL Group) imesherekea sherehe za Uhuru wa Tanganyika, Disemba 9 kwa kufanya usafi katika ufukwe wa Coco Beach kama jinsi alivyoagiza rais wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuagiza kuwa siku ya Uhuru itumike kufanya usafi kutokana na kushamiri kwa uchafu katika mazingira yanayotuzunguka. Kwa kufata agizo hilo la Dkt. Magufuli, MeTL Group kwa kujumuisha viongozi wa kampuni na wafanyakazi wake imefanya usafi kwa pamoja katika ufukwe wa Coco Beach ili kusafisha eneo hilo ambalo linatumiwa na watu wa aina mbalimbali kwenda kujipumzisha pamoja ndugu na familia siku za mapumziko. Hizi ni baadhi ya picha wakati wafanyakazi wa MeTL Group wakifanya usafi katika ufukwe wa Coco Beach; Mkurugenzi wa Masoko wa kampuni ya MeTL Group, Bi. Fatema Dewji-Jaffer (kulia) akiongoza na Afisa Afya wa Manispaa ya Kinondoni, Bw. Kijumbe kuelekea kwenye eneo la usafi mara baada ya kuwasili kwenye fukwe za C...

MAGAZETINI LEO ALHAMISI