SERIKALI KUBORESHA MITAMBO YA KUCHAPISHA NYARAKA YA KIWANDA CHA UHAMIAJI KIJICHI JIJINI DAR ES SALAAM
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba, akizungumza na baadhi ya wananchi waliokuja kupata huduma Makao Makuu ya Idaya ya Uhamiaji wakati wa ziara yake ya siku moja aliyoifanya leo Kurasini jijini Dar es Salaam. Waziri Mwigulu akiwasili kwenye mradi wa ujenzi wa nyumba za makamishna wa Uhamiaji zinazojengwa Kijichi jijini Dar es Salaam kuzikagua. Mrakibu Mwandamizi wa Uhamiaji, Abbas Rovya (kushoto), akimpigia saluti Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba (katikati) kabla ya kukagua nyumba hizo za kisasa. Kulia ni Naibu Kamishna wa Uhamiaji (DCI), Shaban Hamza. Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba (kulia), akiangalia nyaraka mbalimbali zinazochapishwa katika kiwanda cha kuchapa nyaraka za Uhamiaji alipotembelea kiwanda hicho kilichopo Kijichi jijini Dar es Salaam leo. Kutoka kushoto ni Mrakibu Msaidizi wa Uhamiaji (ASP), Singwa Mokiwa na Kaimu Kamishna Generali wa Uhamiaji, Victoria Le...