Skip to main content

Posts

Showing posts from May 31, 2016

MKUTANO WA 12 WA BARAZA LA WADAU WA MAZIWA TANZANIA

Kutoka kushoto ni Msajiili wa Bodi ya Maziwa Tanzania Nelson Kilangozi, Kaimu wa Mwenyekiti wa Baraza la Wadau wa Maziwa Tanzania, Mark Tsoxo, Mwenyekiti wa Baraza la Wadau wa Maziwa Tanzania Dr. Ally Majani, Mwenyekit wa Bodi ya Maziwa Tanzania Aichi Kitalya na mwakilishi kutoka wizarani.  Mwenyekiti wa Baraza la Wadau wa Maziwa Tanzania  Dr. Ally Majani akifungua mkutano wa mwaka wa kumi na mbili (12) wa baraza hilo ,unahusisha wajumbe wote waliochagauliwa toka katika wilaya zote Tanzania  unaofanyika mkoani Njombe, wakati wa maadhimisho ya Kitaifa ya wiki ya Maziwa. Maadhimisho ya wiki ya maziwa kitaifa yanafanyika katika viwaja vya shule ya sekondari Mpechi mkoani Njombe ambapo kesho ni kilele. NJOMBE: Kaimu Mkuu Wa Mkoa Wa Njombe Anatory Choya Amewaagiza Walimu Wa Kuu Na Wakurugenzi Kuanzisha Utaratibu Wa Kufuga Ng'ombe Wa Maziwa Kwa Shule Za Sekondari Na Msingi Ili Wana...

MAANDALIZI YA UTAFITI WA VIASHIRIA NA MATOKEO YA UKIMWI TANZANIA 2016/2017 YAANZA RASMI

Mkurugenzi Mtendaji wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Dkt. Albina Chuwa Akizungumza na wadau wa Utafiti wa Viashiria na matokeo ya Ukimwi wakati wa mkutano wa wadau hao uliofanyika katika ukumbi wa Karimjee leo jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi wa Shirika la Kimataifa linalojishughulisha na masuala ya Afya – ICAP kutoka chuo cha Colombia New youk, Dkt. Fernando Morales akizungumza mbele ya wadau wa Utafiti wa Viashiria na matokeo ya Ukimwi wakati wa mkutano wa wadau ha oleo jijini Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Tume ya Kudhiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS) Bibi. Fatma Mrisho Akizungumza na wadau wa Utafiti wa Viashiria na matokeo ya Ukimwi wakati wa mkutano wa wadau hao uliofanyika katika ukumbi wa Karimjee leo jijini Dar es Salaam. Baadhi ya wadau.  Mkurugenzi Mtendaji wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Dkt. Albina Chuwa wa tatu kutoka kushoto akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa NBS jijini Dar Es Salaam leo. Wito umetolewa kwa wadau pam...

SAKATA LA MAUAJI YA FAMILIYA BILIONEA MSUYA,KAMANDA SIRRO AMDAKA HUYU

Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishina (CP), Simon Sirro akizungumza na waandishi wa habari (hawapo picha) juu ya Jeshi lake kuendelea na operesheni mbalimbali jijini Dar es salaam. Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linamshikiria mtu mmoja kwa tuhuma za mauaji ya Anneth Msuya aliyeuawa kwa kuchinjwa hivi karibuni, Kigamboni wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishina (CP), Simon Sirro amesema kuwa wanamshikilia mtu huyo kwa uchunguzi wa tuhuma za mauaji ya mwanamke huyo. Sirro amesema kuwa katika tukio la mauji ya mwanamke Anneth Msuya polisi wako katika upelelezi na hawezi kutaja jina la mtu wanayemshikilia kutokana na sababu za kiusalama na kuhofea kushindwa kuwakamata watu wengine. Tukio la kuuawa kwa Anneth Msuya lilitokea Mei 26 nyumbani kwake Kibada, Kigamboni ...