Skip to main content

Posts

Showing posts from April 4, 2013

MAMIA YA WAKAZI WA PERAMIHO WAMZIKA MZEE MHAGAMA

  Paroko wa Parokia ya Lugarawa, Jimbo la Njombe Padri Jordan Mwajombe (wa tatu kutoka kushoto) na  Padri Benedict OSB (kulia) wa Parokia ya Peramiho katika Jimbo Kuu la Songea  wakishirikiana kuongoza ibada ya mazishi  leo yaliyofanyika kwenye Jumuyia ya Mtakatifu. Benadetta  Kata ya Peramiho, Songea mkoani Ruvuma.   Watoto wa marehemu Mzee Mhagama wakiweka taji kwa pamoja kwenye kaburi la baba yao wakati  wa mazishi ya yaliyofanyika makaburi ya Lundusi.   Mamia ya wakazi wa Peramiho wakiwa na huzuni kubwa wakati wa mazishi ya aliyekuwa mtumishi wa kiwanda cha uchapaji cha Peramiho, Mzee Bernhard Mhagama katika makuburi ya Lundusi Kata ya Peramiho, Wilaya ya Songea mkoani Ruvuma.

KIWANDA CHA PERAMIHO PRINTING PRESS CHA PATA PIGO

Na Friday Simbaya, Songea Mamia ya wakazi wa Peramiho wilayani Songea mkoani Ruvuma wamzika mfanyakazi wa kiwanda cha uchapishaji cha Peramiho (Peramiho Printing Press), Mzee Bernhard Mhagama (55) katika makaburi ya Lundusi leo (Alhamisi). Mzee Mhagama ambaye pia alikuwa kiungo kikuu katika Kiwanda cha Uchapishaji cha Peramiho katika masuala ya kompyuta alifariki dunia tarehe 02.04.2013 baada ya kuanguka ghafla wakati wakielekea kijiji cha Lugarawa kwenye msiba wa mama yake mzazi, ambapo hata hivyo hawakuwahi mazishi. Ibada ya Misa ya mazishi iliongozwa na Padri Benedict OSB ambaye pia ni Paroko msaidizi wa Parokia ya Peramiho kwa kushirikiana na Paroko wa Parokia ya Lugarawa – Njombe, Pd. Jordan Mwajombe. Akiongea na Nipashe mdogo wa marehemu Beda Mhagama alisema kuwa baada ya kupata taarifa ya misba kwamba mama yao amefariki walifunga safari yeye na marehemu (Mzee Mhagama) pamoja na baadhi ya ndugu, lakini walipofika mjini Njombe kaka yake alizidiwa na kukimbizwa katika h...