Skip to main content

Posts

Showing posts from April 15, 2026

SERIKALI YAWEKA MIKAKATI UJENZI WA SOKO LA MACHINGA IRINGA KUANZA

Na Friday Simbaya, Iringa Serikali imeeleza hatua mbalimbali zinazochukuliwa katika utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Soko la Machinga Complex katika Manispaa ya Iringa, uliopitishwa kwa mwaka wa fedha 2025/2026, ikiwa ni sehemu ya kukabiliana na changamoto ya uhaba wa maeneo rasmi ya kufanyia biashara kwa wafanyabiashara wadogo na wa kati. Akijibu swali la Mbunge wa Iringa Mjini, Fadhili Ngajilo, bungeni, Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi), Festo Dugange, alisema mradi huo unatarajiwa kujengwa katika eneo la zamani la stendi ya mabasi, Kata ya Kitanzini, lenye ukubwa wa mita za mraba 6,555 kwa gharama ya Sh bilioni 4.67. Alifafanua kuwa soko hilo litakuwa na vizimba 800, maduka 150 na migahawa 8, na linatarajiwa kuhudumia wafanyabiashara 958, wakiwemo wafanyabiashara wadogo 800, wa kati 150 pamoja na mama na baba lishe 8. Kwa mujibu wa Dugange, katika mwaka wa fedha 2026/2027, Halmashauri ya Manispaa ya Iringa imetenga Sh milioni 100 kwa ajili ya maandalizi ya ...

POLISI IRINGA WAKAMATA WATUHUMIWA 53, WAONYA TAARIFA ZA UONGO

Na Friday Simbaya, Iringa Jeshi la Polisi Mkoa wa Iringa limekamata jumla ya watuhumiwa 53 kwa makosa mbalimbali ya uhalifu katika operesheni zilizofanyika maeneo tofauti kuanzia Aprili Mosi, 2026, huku likitoa onyo kali kwa wananchi dhidi ya utoaji wa taarifa za uongo zinazosababisha taharuki. Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, SACP Allan Bukumbi, alisema miongoni mwa waliokamatwa ni Ramadhani Mussa (33), dereva mkazi wa Dar es Salaam, aliyetiwa hatiani kwa kosa la kutoa taarifa za uongo kuwa ameibiwa sehemu zake za siri. Kwa mujibu wa Bukumbi, mahakama ilimhukumu Mussa kifungo cha miaka mitano jela baada ya kuthibitika kuwa taarifa aliyotoa haikuwa ya kweli. “Katika operesheni hizi, tumefanikiwa pia kuwakamata watu wengine waliokuwa wakitoa taarifa za uongo na kusababisha taharuki kwa wananchi,” alisema Bukumbi. Aliwataja watuhumiwa wengine kuwa ni Mussa Kaundi (39), mfanyabiashara mkazi wa Mafinga, pamoja na wenzake wawili kutoka Isakalilo, M...

Kikao Kazi Cha Kuandaa Mpango Wa Mkoa Wa Afya Moja Kilichoratibiwa Na Ofisi Ya Waziri Mkuu

Baadhi ya wataalam wakiwa katika kazi za vikundi wakati wa kikao kazi cha kuandaa Mpango wa Mkoa wa Afya Moja kilichoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) Sehemu ya Afya Moja kwa kushirikiana na Shirika lisilo la Serikali la CIHEB Tanzania kupitia Mradi wa Usalama wa Afya Duniani.Kikao kimefanyika katiks ukumbi wa mikutano wa Korogwe Executive Hotel katika Halmashauri ya Mji wa Korogwe mkoani Tanga, tarehe 15 Aprili, 2026. Baadhi ya Wataalam cha kuandaa Mpango wa Mkoa wa Afya Moja wakiwasilisha kazi za vikundi wakati wa kikao kazi cha kuandaa Mpango wa Afya Moja kwa Mkoa wa Tanga. Kikao hicho kilichoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu) Sehemu ya Afya Moja kwa kushirikiana na Shirika lisilo la Serikali la CIHEB Tanzania kupitia Mradi wa Usalama wa Afya Duniani na kufanyika katika Halmashauri ya Mji wa Korogwe mkoani Tanga, tarehe 15 Aprili, 2026. Picha ya pamoja ya wataalam wa masuala ya Afya Moja waliokutana kuandaa...