Na Friday Simbaya, Iringa Serikali imeeleza hatua mbalimbali zinazochukuliwa katika utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Soko la Machinga Complex katika Manispaa ya Iringa, uliopitishwa kwa mwaka wa fedha 2025/2026, ikiwa ni sehemu ya kukabiliana na changamoto ya uhaba wa maeneo rasmi ya kufanyia biashara kwa wafanyabiashara wadogo na wa kati. Akijibu swali la Mbunge wa Iringa Mjini, Fadhili Ngajilo, bungeni, Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi), Festo Dugange, alisema mradi huo unatarajiwa kujengwa katika eneo la zamani la stendi ya mabasi, Kata ya Kitanzini, lenye ukubwa wa mita za mraba 6,555 kwa gharama ya Sh bilioni 4.67. Alifafanua kuwa soko hilo litakuwa na vizimba 800, maduka 150 na migahawa 8, na linatarajiwa kuhudumia wafanyabiashara 958, wakiwemo wafanyabiashara wadogo 800, wa kati 150 pamoja na mama na baba lishe 8. Kwa mujibu wa Dugange, katika mwaka wa fedha 2026/2027, Halmashauri ya Manispaa ya Iringa imetenga Sh milioni 100 kwa ajili ya maandalizi ya ...
Pamlomo-Sauti Ya Jamii (SYJ) is essentially a digital news platform that shares different types of news updates — social, political, economic, sports, entertainment, and community stories. From the context you’ve given, it is based in Iringa, Tanzania, and functions mainly as an online outlet (likely through social media such as Facebook, YouTube, or other channels) where audiences can get real-time updates.