Skip to main content

Posts

Showing posts from September 1, 2014

Msigwa atoa mifuko 100 Kata ya Nduli

Na Mathias Canal, Kwanza Jamii Mbunge wa Iringa Mjini Mch Peter Simon Msigwa ametoa mifuko 100 ya Saruji kumalizia shule ya Sekondari Nduli ili kupunguza usumbufu mkubwa wanaoupata wananchi wa Kata hiyo kwani wanafunzi wamekuwa wakiteseka kusoma mbali na kijiji hicho. Amesema kuwa tofauti za kisiasa kati yake na Diwani wa Kata hiyo zimemalizika badala yake ni muda wa kufanya shughuli za maendeleo.

SEMINA ya Mafunzo ya Mchezo wa Mpira wa Mikono IRINGA

Mwalimu wa shule ya manguajuki singida, Mataka Juma akichangia mada wakati mafunzo ya Handball yanayoendelea mjini Iringa Mwalimu ya mchezo wa mpira wa mikono ambaye pia ni mwenyekiti kamati ya ufundi Chama cha Mpira wa Mikono Taifa, (Chairman Technical Committee of Tanazania Amateur Handball Association), (TAHA),David kiama akiwaonesha washiriki namna kiwanja cha mchezo huo unavyoonekana wakati mafunzo yanayoendelea mjini Iringa. (PICHA NA FRIDAY SIMBAYA)