Skip to main content

Posts

Showing posts from November 2, 2014

IGP MSTAAFU PHILEMONI MGAYA ASHEREHEKEA MIAKA 85 YA KUZALIWA

Mara Baada ya Ibada katika Kanisa la Azania Front wakati wa kuadhimisha miaka 85 ya kuzaliwa ya aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Philemoni Mgaya Baadhi ya waumini mbalimbali wakiwa nje baada ya Ibada Mkuu  wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Mstaafu Philemoni Mgaya akiwa katika siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwake 

CHADEMA WAENDELEA KUHAMASISHA WANANCHI KUHUSU UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA

Katibu wa  CHADEMA  Wilaya ya Iringa mjini Suzan Mgonokulima (katikati) akihutubia wananchi wa  Mtaa wa Mwangata D eneo la Mapekosi katika Kata  ya Mwangata wakati mkutano wa hadhara uliofanyika leo jioni wenye lengo la kuhamasisha wananchi kujitokeza na kugombea nafasi za uongozi kama vile uwenyekiti na ujumbe  katika mtaa huo hasa akinamama. Baadhi ya wakazi wa Mtaa wa Mwangata D wakijitokeza kujiandikisha majina kwa mmoja ya viongozi wa CHADEMA ili kuweza kushiriki katika mchakato wa kumpata mwenyekiti wa mtaa pamoja na wajumbe 6 kupitia chama hicho na hatimaye kuweza kushindanishwa na vyama vinge vya siasa vitakavyosimamisha wagombea wao wakati wa uchaguzi wa serikali za mitaa hapo tarehe 14 Desemba mwaka huu.

MAGAZETI LEO JUMAPILI

. . .

THE QUESTION OF POWER; EDGAR LUNGU FINALLY SPEAKS

"You see, King Solomon in his wisdom was encountered by two women. One was claiming ownership of a child and the other was doing the same. The King then asked for a sword to split the child in two. At that point, the real mother apologised and gave up the child. This is just an example of where we are.

NEEMA CRAFTS WATOA MSAADA WA BASKELI KWA WALEMAVU

Walemavu Mkoani Iringa wakifurahia baada ya kukabidhiwa baskeli zao ikiwa ni msaada kutoka Neema Crafts Mkurugenzi Mtendaji wa Neema Crafts Bwana Benjamin Ray akitoa ufafanuzi juu ya msaada wa baskeli walioutoa kwa walemavu wa Mkoani Iringa.   Na Simon Victor Walemavu mbalimbali mkoani Iringa hapo jana walipewa msaada wa baskeli arobaini (40) kutoka Neema Crafts ambao wako chini ya dayosisi ya Ruaha.

WAZIRI WA AFYA MH. SEIF RASHIDI AZINDUA RASMI GHETTO RADIO

Waziri wa Afya Mh. Seif Rashid akiongea na Wauguzi wa Hospitali teule ya Mkoa wa Temeke, Wafanyakazi wa Ghetto Radio ya Sibuka Fm pamoja na wadau mbalimbali wakati wa uzinduzi Rasmi wa Radio hiyo, ambayo lengo lake ni kuwakomboa vijana wa Mtaani pamoja na vipindi vingine vya kuelimisha Jamii na Burudani, Pia amewashukuru kwa kutoa msaada wa vifaa mbalimbali ambavyo vitasaidia katika Hospitali.  Mkurugenzi wa Sibuka George Ndagali akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa Ghetto Radio ya Sibuka Fm iliyo fanyika katika  katika Hosipitali Teule ya Mkoa wa Temeke Ambapo Ghetto Radio Imeweza kufunguliwa Rasmi Katika Mkoa huo nakuweza kutoa Msaada Vifaa Mbalimbali pamoja na Madawa Ambavyo Vyote kwa ujumla vimegharimu kiasi Cha Shilingi Milioni sita na Laki sita.  Mkurugenzi wa Ghetto Radio Matt Brouwer akizungumza neno wakati wa uzinduzi wa Ghetto Radio ya Sibuka Fm Ambapo Bw.Brouwer Alisema kuwa Ghetto Radio ilianzishwa nchini Kenya Miaka Sita iliyopita n...

JK AONGOZA WAOMBOLEZAJI KUAGA MWILI WA MAREHEMU MEJA JENERALI AIDAN ISIDORE

Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisaini kitabu cha  Maombolezo wakati wa kuaga mwili wa Marehemu Meja Jenerali Aidan  Isidore Mfuse katika hospitali kuu ya JWTZ ya Lugalo jijini Dar es  slaam jana kabla ya mwili huo kusafirishwa kwenda  Njombe kwa mazishi yanayotarajiwa kufanyika leo Jumapili Novemba 2, 2014 Rais Mstaafu Mhe Benjamin William Mkapa akitoa heshima za mwisho  wakati wa kuaga mwili wa Marehemu Meja Jenerali Aidan Isidore Mfuse  katika hospitali kuu ya JWTZ ya Lugalo jijini Dar es slaam jan  kabla ya mwili huo kusafirishwa kwenda Njombe kwa mazishi  yanayotarajiwa kufanyika leo Jumapili Novemba 2, 2014

SERIKALI ITAENDELEA KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA KWA WANANCHI-DKT.BILALI

Na Frank Mvungi-MAELEZO Serikali imesema itaendelea kuboresha huduma za afya hapa nchini kuanzia ngazi ya Zahanati hadi Hosipitali za Rufaa zote nchini ili kuhakikisha wananchi wanapata matatibu bora na yanayoridhisha. Kauli hiyo imetolewa hivi karibuni jijini Dar es salaam na Makamu wa Rais Dkt. Mohamed Gharib Bilali wakati akifungua Kongamano la wadau wa Afya nchini.

UN YAOKOA MAISHA YA WATOTO 3000 ZANZIBAR

Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akizungumza na waandishi wa habari wa Zanzibar kwenye ofisi ndogo za mashirika ya Umoja wa Mataifa visiwani Zanzibar kuhusiana na mafanikio ya mradi wa kusaidia maendeleo nchini Tanzania (UNDAP) ulioanza mwaka 2011 na sasa ukiwa ukingoni. Kulia ni Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues na kushoto ni Mtaalam wa Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania, Hoyce Temu.

Watahiniwa 11,781 mtihani wa kidato cha nne kufanya mtihani mkoa wa Iringa

Ofisa Elimu Mkoa wa Iringa, Joseph Mnyikambi akiongea na waandishi wa habari jana ofisini kwaka. (PICHA NA FRIDAY SIMBAYA) Na Friday Simbaya, Iringa MITIHANI ya wanafunzi wa kidato cha nne na maarifa (Qualifying Test) kitaifa unatarajia kufanya nchini kote hapo tarehe 3 Novemba mwaka huu.