Skip to main content

Posts

Showing posts from October 4, 2011

MWANAFUNZI ULAYASI AFUKUZWA SHULE BAADA YA KUFUMANIWA NA MWANAUME VICHAKANI WAKIFANYA MAPENZI

Na Friday Simbaya, Ludewa IKIWA imebaki siku moja tu kuanza kwa mtihani wa Taifa wa Kidato cha nne nchini mwanafunzi Hosana Raaban wa Shule ya Sekondari Ulayasi Ludewa mkoani Iringa ametimuliwa shule baada ya kukamatwa na walimu wake akifanya mapenzi na mwanaume vichakani kinyume na sheria za shule. Mwanafunzi Hosana Raaban (20) anayetoka katika Kijiji cha Ligumbilo katika Kata ya Mlangali alikutwa na mkasa huo Oktoba 2 mwaka huu katika vichaka vinavyoizunguka shule hiyo baada ya kuwatoroka walimu waliokuwa wakisubiri kwa vifaa vya mitihani shuleni hapo tayari kwa mtihani kesho yake. Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Bw Richard Chitundu akizungumza kwa njia ya simu alikiri kutokea kwa fumanizi hilo vichakani majira ya saa kumi na moja jioni na kukiri kosa  na kutakiwa kufika kesho yake akiwa ama na mzazi au mlezi wake ili kupata ufumbuzi wa suala hilo, lakini mwanafunzi na wazazi wamekaidi agizo hilo. Akielezea tukio lenyewe Bw Chitundu...