Skip to main content

Posts

Showing posts from May 8, 2017

ANSGAR CUP 2017 PERAMIHO, NGOMA 'INOGILE'

Na Alex Mapunda, Ruvuma MWAKILISHI wa Kata ya Peramiho katika Mashindano ya Ansgar Cup ngazi ya Tarafa, timu ya Afya Fc imefanikiwa kuitandika bila huruma Kilagano Fc timu toka Kata ya Kilagano kwa kichapo cha bao 3-0. Katika mchezo huo ambao Mgeni rasmi alikuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Simon Bulenganija, bao la kwanza la Afya Fc liliwekwa kimiani na mshambuliaji machachari Emanuel Kajana dakika ya 39 ambalo liliwachanganya wachezaji wa Kilagano FC na wakaanza kucheza kwa Tahadhari kubwa. Dakika 15 za kipindi cha pili Kilagano Fc walicheza vizuri mno na walifanikiwa kufanya mashambulizi ya mara kwa mara katika lango la Afya Fc, lakini mambo yalikuwa tofauti baada ya mchezaji wa Afya Fc Shabiru Kinunga kuipatia timu yake hiyo bao la pili lililopeleka majonzi kwa Kilagano Fc mnamo dakika ya 60 ya mchezo. Lakini Kabla ya mpira kumalizika mfungaji wa bao la kwanza Emanuel Kajana alishindilia msumari wa moto katika vidonda vya Kilagano Fc...

NHIF TANGA KUPELEKA HUDUMA YA TOTO AFYA KADI VIJIJINI

MFUKO wa Taifa wa Bima ya Afya mkoani Tanga (NHIF) unakusudia kuwafikia wananchi kwenye vijiji na kata mbalimbali mkoani hapa ili kutoa elimu juu ya umuhimu wa huduma ya afya kwa watoto (Toto Afya Kadi) ambapo uelewa wake umekuwa sio mzuri. Hayo yalisemwa na Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Tanga (NHIF) Ally Mwakababu (Pichani Juu)wakati akizungumza na mtandao huu ofisini kwake ambapo alisema wameamua kufanya hivyo ili kuipa uelewa jamii kuhusiana na umuhimu na faida za huduma hiyo. Alisema wakiwa huko watapita kwenye maeneo mbalimbali ikiwemo mashuleni na kufanya mikutano ya nje kwa wananchi ili kuweza kuwapa uelewa juu manufaa ya kuwaingiza watoto hao kwenye mfuko huo. “Unajua hii huduma Toto Afya Kadi hasa kwa maeneo ya vijijini uelewa wake umekuwa sio mzuri hivyo sisi tumepanga kuanza kuhamasisha na kuipa uelewa jamii ili waweze kuitambua na kujiunga nayo “Alisema. “Nia kubwa ni kutaka kuona jamii waliochini ya miaka 18 wana jiunga na Mfu...