Skip to main content

Posts

Showing posts from August 3, 2011

WAFANYABIASHARA SOKO KUU LUDEWA WAMETELEKEZWA VYOO VICHAFU, HAVINA MAJI SOKO HALINA ULINZI.

Wengi sasa wafanyia biashara mtaani na majumbani. WAKATI Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa ikilalamikia ufinyu wa Bajeti na kushindwa kutekeleza miradi ya maendeleo na huduma muhimu za jamii kwa kukosa raslimali fedha, wafanyabiashara katika soko kuu la mjini hapa wamelikimbia soko na kuamua kufanyia majumbani bila kulipa ushuru kutokana na soko hilo kukosa huduma muhimu za kiutu kama vile choo safi, maji na mlinzi. Wakizungumza katika soko jipya wafanyabiashara wa mbogamboga, nyanya, vitunguu na matunda walisema wanalazimika kukimbilia majumbani kwao hata kama ni mbali kwa ajili ya kwenda kujisaidia kutoka na soko hilo kuwa na vyoo vichafu vya zamani huku soko jipya nalo likikosa maji wakati vyoo ni vya kuflashi. ”Ndugu mwandishi hebu angalia na uingie wewe mwenyewe ndani ya vyoo hivyo kama unaweza kujisaidia na kuvumilia hali ya uchafu kila siku tunalazimika kwenda majumbani kujisaidia na kisha kurudi kuendelea na biashara.ni hatari sana inasikitisha,” alisema mmoja wa wafanyabiashara ...

MALKIA WA MCHWA HUYU HAPA

  Matola Suleiman mkazi wa Songea Mahenge katika Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma akiwa ameshika malkia wa mchwa mkononi kutoka kwenye shimo alikojificha chini ya sakafu ya nyumba ya mkazi wa Peramiho leo. Sulemani ambaye ni mwenyeji wa Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma alisema alianza kazi ya kutoa mchwa tangu 1980. Tatizo la mchwa ni kubwa katika Mkoa wa Ruvuma.   Shimo alimopatika Malkia wa mchwa ili hapa.   Malkia wa mchwa  jinsi anavyoonekana vizuri. Pembeni mwa malkia wa mchwa ni kadume ka malkia.

DC LUDEWA ACHANGISHA MILIONI 5 ZA UJENZI WA SHULE NA KUSEMA LUDEWA WAGUMU KUCHANGIA ELIMU WEPESI KWENYE SHEREHE.

MKAMATE elimu usimwache aende zake maana yeye ni uzima wako, na kama unadhani elimu ni gharama basi, jaribu ujinga. Hiyo ni kauli mbiu iliyotumika jana katika Harambee ya kuchangia ujenzi wa shule ya Sekondari ya Matakatifu Alois inayomilikiwa na Kanisa Katoliki Jimbo la Njombe, Parokia ya Ludewa. Mkuu wa Wilaya ya Ludewa Bi. Georgina Bundala kama mgeni rasmi akiwakilishwa na Afisa Maaendeleo ya Jamii Wilaya Bw. Lazaro Mapunda aliongoza harambee hiyo iliyohudhuriwa na wadau na wananchi wachache lakini akafanikiwa kuchangisha jumla na zaidi ya shilingi 5m/- na kuungwa mkono na wageni kutoka makao makuu ya Jimbo Katoliki la Njombe. Wananchi wilayani Ludewa wanatakiwa kushiriki na kuwekeza zaidi katika elimu ili kuongeza idadi ya wataalamu wilayani humo na Taifa kwa ujumla badala ya kupoteza muda na fedha nyingi kwenye vikao vya harusi na sherehe zingine zinazohusiana na mambo ya burudani,kuselebuka, kulakula na kunywa huku watoto wakiendelea kufanya vibaya katika mitihani yao. Hayo ...