Skip to main content

Posts

Showing posts from January 25, 2017

MADC WATEMBELEA SHAMBA LA JARIBIO LA MAHINDI LA KITUO CHA MAKUTUPORA

Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais-Muungano na Mazingira, Profesa Faustine (kushoto), akizungumza na wakuu wa wilaya za Dodoma na maofisa watendaji na wenyeviti wa serikali za mitaa na wadau wa kilimo alipotembelea shamba la Jaribio la Mahindi yaliyoboreshwa kwa kutumia Teknolojia ya Uhandisi Jeni (GMO) chini ya Mradi wa Mahindi Yanayostahimili Ukame (WEMA) katika Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Makutupora mkoani Dodoma leo. Wakuu wa Wilaya za Mkoa wa Dodoma wakiwa kwenye mkutano na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais-Muungano na Mazingira, Profesa Faustine (hayupo pichani), walipotembelea Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Makutupora mkoani Dodoma leo. Kutoka kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, Deogratius Ndejembi, Bahi, Elizabeth Kitundu, Mpwapwa Jabir Shekimweri na Mshauri wa Kilimo Ofisi ya Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma, Aziza Mumba. Mkurugenzi wa Utafiti na Maendeleo wa Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi, Hussein Mansour akizungumza (kushoto), akiwaelekeza ja...

VIONGOZI WA VIJIJI WAHOFIA UTEKELEZAJI WA KODI YA MAJENGO

Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesela akizungumza na wenyeviti wa vijiji, watendaji wa vijiji, watendaji wa kata, tarafa pamoja na wakuu wa idara wa halmashauri ya Wilaya ya Iringa  kuhusu utekelezaji wa kodi ya majengo kwa vijiji wakati wa kikao cha kazi kilichofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Iringa jana. (PICHA NA FRIDAY SIMBAYA) Mwenyekiti wa Kijiji cha Mahuninga, Kata ya Mahuninga wilayani Iringa, mkoani Iringa Lonjino Mkwele akimuuliza swali Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard Kasesela (hayupo pichani) kuhusu utekelezaji wa kodi ya majengo kwa vijiji wakati wa kikao cha kazi kilichofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri ya Iringa jana. (PICHA NA FRIDAY SIMBAYA) VIONGOZI wa vijiji vyote wa Wilaya ya Iringa, mkoani Iringa waagizwa kusoma mapato na matumizi ili kuwarahisishia wananchi kufahamu jinsi fedha zao zinavyotumika na kutoa fursa kwa wananchi kupata nafasi ya kuhoji ili kujiridhisha pale wanapokuwa na mashaka. Agizo hil...