Skip to main content

Posts

Showing posts from August 13, 2011

DKT MFUTAKAMBA: ZAIDI YA BILIONI 6 KUBORESHA USAFIRI WA MELI ZIWA NYASA,V ICTORIA NA TANGANYIKA

LUDEWA              SERIKALI imetenga zaidi ya shilingi bilion 6 kwa ajili ya kuboresha usafiri wa Meli katika maziwa matatu nchini likiwemo Ziwa Victoria, Ziwa Tanganyika na Ziwa Nyasa ambalo ni ziwa pekee lenye kero na changamoto kwa wananchi wa Ludewa, Songea na Mbeya. Hayo yalisemwa na Naibu Waziri wa Uchukuzi Dkt Athumani Mfutakamba alipotembelea Kata ya Masasi na Manda Wilayani Ludewa kujionea mwenyewe eneo kitakapojengwa kiwanja cha ndege katika kijiji cha Sagalu kama njia ya kuvutia wawekezaji kufika na kuwekeza Wilayani humo. Dkt Mfutakamba alisema kuwa ujenzi wa uwanja wa ndege Sagalu Wilayani Ludewa utasaidia kwa kiasi kikubwa kukuza uchumi na kufungua milango ya kimaendeleo zaidi wilayani humo kutokana na kuwa na utajiri wa madini ya chuma na makaa ya mawe na dhahabu. Hata hivyo waziri huyo aliahidi kuwa ujenzi wa uwanja huo muhimu ...

DIWANI LUDEWA AMKANA DC MKUTANONI, AGEUKA BUBU KUJIBU MASWALI LIKIWEMO LA KUMFUKUZA MWANDISHI WA HABARI

Na Friday Simbaya, Ludewa DIWANI wa Kata ya Ludewa ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludew, Bi Monica Mchiro juzi alimkana hadharani Mkuu wa Wilaya hiyo Bi Georgina Bundala kutokana na mkuu huyo kutokuweka bayana kilichotokea kati ya wananchi na watafiti wa madini walioingia na mitambo na kuanza shughuli katika Kata ya Iwela bila taarifa kwa madiwani na kuzua hofu na mkanganyiko kwa wananchi. Bi Monica alifikia hatua hiyo ya kuwaambia wananchi ukweli baada ya Naibu Kamishna wa Madini Kanda ya Mbeya Bw. John Shija kuweka wazi Sheria za Madini na jinsi walivyotekeleza baada ya kutoa leseni ya utafiti katika kata ya Iwela na hatimaye wananchi kugundua kuwa tatizo lilikuwa katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi. Bi. Monica pamoja na wapigakura wake walikuwa wametega masikio na kutegemea kuwa Mkuu wa Wilaya hiyo Bi Georgina Bundala angetoa ufafanuzi juu ya utata ul...