Skip to main content

Posts

Showing posts from February 18, 2018

FAMILIA YA MKAZI MMOJA WA MANISPAA YA IRINGA YANUSURIKA KUNGUA MOTO

Na Friday Simbaya, Iringa  Familia ya mkazi mmoja wa Mwangata Msikitini katika kata ya Mwangata Manispaa ya Iringa yanusurika kuteketea kwa moto baada ya majirani kuwaokoa kwa kufumua dirisha la nyuma ya nyumba yao.  Tukio hilo limetokea majira ya saa 5:30 asubuhi wakati famila ya onesmo cosmas ikiwa ndani wakiendelea na shughuli ambapo chanzo za moto kinadaiwa ni mtungi wa gesi kuvuja.  Mwandishi wa gazeti la Nipashe alishuhudia wananchi wakihangaika kuzima moto kwa kutumia mipira ya maji na ndoo pamoja na mchanga ambapo hatimaye uliwashinda na kuomba msaada kutoka jeshi la zimamoto.  Baadhi ya mashuhuda walioongea na Nipashe jana walisema kuwa wamepiga simu ya dharura ya zimamoto ambayo ni 114 kuwajulisha tukio la moto ambapo walisema gari la zimamoto na uokoaji lilifika kwa kuchelewa baada ya muda na kuudhibiti moto kabla haujashika nyumba nyingine za jirani  Shuhuda wa ajali ya moto Musa Juma ambaye ni mkazi wa Kata y...