Skip to main content

Posts

Showing posts from March 23, 2016

Mashambulizi ya kigaidi ya Brussels

Mashambulizi yaliyotokea jana katika mji mkuu wa Ubelgiji, Brussels yameendelea kuakisiwa na kulaaniwa sana katika vyombo vya habari na duru za kimataifa. Baada tu ya mashambulizi hayo yaliyolenga uwanja wa ndege wa Zaventem mjini Brussels na kituo cha treni ya chini kwa chini, Baraza la Usalama wa Taifa la Ubelgiji lilikutana na kujadili kadhia hiyo. Takwimu zinasema kuwa, hadi sasa watu wasiopungua 34 wameuawa katika mashambulizi hayo na wengine zaidi ya 190 kujeruhiwa. Kundi la kigaidi la Daesh limetangaza kuwa limehusika na mashambulizi hayo. Mashambulizi ya kigaidi yaliyotokea jana mjini Brussels yanafuatia yale yaliyotokea Paris, Ufaransa miezi ya Januari na Novemba mwaka jana. Mashambulizi hayo kwa mara nyingine tena yamepiga kengele ya hatari kwa viongozi wa masuala ya kisiasa na kiusalama juu ya tishio kubwa la makundi ya kigaidi na kitakfiri barani Ulaya. Siku kadhaa zilizopita askari usalama wa Ubelgiji walimtia nguvuni Salah Abdulsalam ambaye inasemeka...

Nguesso ashinda uchaguzi wa rais Congo Brazaville

Matokeo ya awali ya uchaguzi wa rais huko Jamhuri ya Congo Brazaville yanaonyesha kuwa Rais Denis Sassou Nguesso anaongoza kwa wingi wa kura. Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi nchini humo Henri Bouka, amesema Rais Sassou Nguesso anaongoza kwa asilimia 67 ya kura zote halali zilizopigwa katika uchaguzi uliofanyika Jumapili. Hata hivyo wagombea watano wa kiti cha rais wamesema hawatambui matokeo hayo. Itakumbukwa kuwa, serikali ya Congo Brazzavile iliyaagiza mashirika mawili makubwa ya simu nchini humo ya MTN Congo na Airtel Congo kukata mawasiliano yote ya simu wakati wa kufanyika zoezi la uchaguzi wa Rais. Aidha serikali ilisitisha huduma za intaneti katika kipindi hicho. Waziri wa Mambo ya Ndani wa Congo Brazzavile aliziambia duru za habari kwamba, uamuzi huo wa kukatwa mawasiliano ya simu na intaneti umechukuliwa kutokana na sababu za kiusalama. Rais Nguesso ambaye ameingoza nchi hiyo kwa zaidi ya miaka 30, Oktoba mwaka jana alibadilisha katiba na kuondoa kipengee ...

Tigo yatoa 300m/- kudhamini wanafunzi wa tehama vyuo vikuu

Meneja mkuu wa Tigo, Diego Gutierrez akiongea na waandishi wa habari(hawapo pichani)wakati wa kutangaza udhamini wa kampuni hiyo kwa  wanafunzi tisa wanaochukua mafunzo ya Tehama katika vyuo vikuu vya hapa wa jumla ya shilingi million 300 mapema leo  jijini Dar Es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi mkuu wa DTBi, Mhandisi George Mulamula na kushoto ni Meneja wa huduma za Jamii Tigo, Woinde Shisael. Mkurugenzi mkuu wa DTBi, Mhandisi George Mulamula  akiongea na waandishi wa habari(hawapo pichani) katikati ni  Meneja mkuu wa Tigo, Diego Gutierrez, na kushoto ni Meneja wa huduma za Jamii Tigo, Woinde Shisael.  wakati wa kutangaza udhamini wa kampuni hiyo kwa  wanafunzi tisa wanaochukua mafunzo ya Tehama katika vyuo vikuu vya hapa wa jumla ya shilingi million 300 mapema leo  jijini Dar Es Salaam. Meneja mkuu wa Tigo, Diego Gutierrez   akipeana mkono na  Mmoja wa wanafunzi waliopata udhamini wa tigo  Carolyne Paul, mwanafunzi w...