Mkuu wa Fedha na Tahadhari wa Huduma ya Fedha kwa njia ya mtandao Tigo, Obedi Laiser akielezea kuhusu gawio la mwaka huu kwa watumiaji wa Tigo Pesa, kushoto kwake ni Meneja wa Mawasiliano, John Wanyancha Waandishi wa habari wakisikiliza kwa makini maelezo kuhusu gawio la mwaka huu la tigo pesa katika mkutano uliofanyika mapema leo katika makao makuu ya Tigo Kijitonyama Dar es salaam. Mkuu wa Fedha na Tahadhari wa Huduma ya Fedha kwa njia ya mtandao Tigo, Obedi Laiser akijibu maswali ya waandishi wa habari (Hawapo pichani) kuhusu gawio la mwaka huu kwa watumiaji wa Tigo Pesa, kushoto kwake ni Meneja wa Mawasiliano, John Wanyancha Dar es Salaam, Januari 13, 2016- Kampuni inayongoza katika kuleta maisha ya kidijitali kwa jamii, Tigo, imetangaza tena malipo ya robo mwaka ya shilingi bilioni 4.4 (dola milioni 2.1) kwa watumiaji wake wa huduma ya Tigo Pesa wapatao milioni 4.6. “Gawio hili la faida linalipwa kwa watumiaji wote wa Tigo Pesa wakiwemo wateja binafsi, mawakala wa r...