Skip to main content

Posts

Showing posts from June 9, 2017

INTANETI INAVYOCHOCHEA UKUAJI WA UTALII BARANI AFRIKA

Na Jumia Travel Tanzania Afrika ni bara la pili kwa kuwa na idadi kubwa ya watu ambapo inafikia takribani bilioni 1.2 (wengi wao wakiishi mijini) na inatarajiwa kongezeka mpaka bilioni 2.5 kufikia mwaka 2050 (25% ya watu wote duniani). Kwa mujibu wa ripoti ya utalii kwa Afrika mwaka 2017 iliyofanywa na Jumia Travel imebainisha kwamba mtu mmoja kati ya watatu ni sehemu ya watu wa daraja la kati (watu wanaofanyakazi kwenye taaluma na biashara mbalimbali pamoja na familia zao) na wanatarajiwa kuongezeka mara mbili zaidi kufikia 2050. Watu wa daraja la kati ni muhimu katika uchangiaji wa ukuaji wa utalii wa ndani na ukanda mzima tuliopo. Miongoni mwa mambo yanayochochea maendeleo na ukuaji wa sekta mbalimbali Afrika ikiwemo utalii ni pamoja na mtandao wa intaneti. Mpaka hivi sasa, watumiaji wa mtandao wa intaneti barani Afrika wamefikia zaidi ya milioni 300, ambayo ni sawa na 9.3% ya waafrika wote na 27.7% ya ueneaji wake. Kwa kiasi kikubwa idadi hiyo imecha...

WAKINA BABA WATAKIWA KUTOA ELIMU YA AFYA YA UZAZI KWA WATOTO WAO

Ofisa Programu wa TGNP Mtandao, Anna Sangai (kushoto), akitoa mada katika kongamano la siku moja lililohusu elimu ya afya ya uzazi lililofanyika Makao Makuu ya TGNP Mabibo Dar es Salaam jana. Kongamano hilo liliandaliwa na TGNP. Mwanafunzi Leila Kisinga kutoka Sekondari ya Mabibo akitoa mada kuhusu via vya uzazi vya mwanamke vinavyofanya kazi. Kongamano likiendelea. Mshiriki Idd Hamisi akichangia jambo katika kongamano hilo. Usikivu katika kongamano hilo. Aisha Kijavara akichangia. Wakina mama wakiwa katika kongamano hilo. Wakina mama hao walitoa uzoefu wao kuhusu afya ya uzazi kwa watoto. Mwanafunzi Juma Nasoro kutoka Sekondari ya Mabibo akitoa mada kuhusu via vya uzazi vya mwanaume vinavyofanya kazi. Mdau Selemani Bishagazi akichangia kuhusu wanaume kuwasaidia watoto wao wa kike wanapokuwa katika hedhi. Mary Mbarawa akichangia jambo. Na Dotto Mwaibale WAKINA Baba nchini...

RC ANNA MNGWIRA ATEMBELEA FAMILIA YA DKT NDESAMBURO,AZUNGUMZA NA WANACCM

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Anna Mngwira akizungumza na baadhi ya viongozi wa Chama cha Mapinduzi alipotembelea ofisi za chama hicho kujitamburisha .kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi mkoa wa Kilimanjaro Idd Juma ,na anayefuatia ni Katibu tawala mkoa wa Kilimanjaro Mhandisi,Aisha Amour. Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Manispaa ya Moshi,Elizabeth Minde (katikati) akifurahia jambo wakati Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Mngwira (hayupo pichani) alipokutana na uongozi wa chama hicho katika ofisi za CCM-Mkoa wa Kilimanjaro. Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kilimanjaro ,Idd Juma akitoa neon la shukrani mara baada ya Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro ,Anna Mngwira kutembelea ofisi za chama hicho. Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Mngwira akitoka ofisi za Chama cha Mapinduzi mkoa wa Kilimanjaro mara baada ya kuonana na viongozi wa chama hicho. Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ,Anna mngwira akisalimaiana na Katibu wa Chama cha Demokrasia...