*Kila Alhamisi wakuu wa Wilaya, wakuu wa idara kwenda vijijini Na Gordon Kalulunga, Mbeya MKUU wa mkoa wa Mbeya, Amos Makala, amekabidhiwa rasmi ofisi yake leo na aliyekuwa Mkuu wa mkoa huo Abbas Kandoro, huku akitoa maagizo manne mazito kwa watumishi wa serikali. Makala alisema kuwa, wakuu wote wa wilaya na wakuu wa idara katika Halmashauri za wilaya zilizopo mkoa wa Mbeya, kila siku ya Alhamisi kuanzia saa nne mpaka saa nane mchana ni marufuku kukaa ofisini bali wanatakiwa kwenda kupokea kero za wananchi vijijini na kuzishughulikia. “Mimi sijaja kutengua torati bali kutimiliza. Kila mmoja wetu atimize wajibu wake na kuacha vyeo vya uadmin wa magroup kwenye Whats App na face book” alisema Makala. Alisema agizo lingine hataki kusikia masuala ya ugonjwa wa kipindupindu katika Halmashauri za mkoa wa Mbeya, huku akiagiza kuwa lazima mazingira yawekwe safi. Kuhusu watumishi hewa wanaolipwa mishahara alisema jambo hilo halihitaji digrii ili kuelewa...
Pamlomo-Sauti Ya Jamii (SYJ) is essentially a digital news platform that shares different types of news updates — social, political, economic, sports, entertainment, and community stories. From the context you’ve given, it is based in Iringa, Tanzania, and functions mainly as an online outlet (likely through social media such as Facebook, YouTube, or other channels) where audiences can get real-time updates.