WANANCHI WENYE HASIRA LUGARAWA WAKATA MABOMBA YA MAJI YA PAROKO, NI BAADA YA MWENYEKITI WAO KUMPIGIA MAGOTI BILA MAFANIKIO.
LUDEWA
WANANCHI na watumiaji wa maji katika
Kitongoji cha Luafyo Juu Lugarawa wilayani Ludewa jana walijawa jazba na kuamua
kuyakata kwa mapanga mabomba ya maji yanayotumika pia na Kanisa Katoliki kwa
madai kuwa Paroko wao amewanyima maji bila sababu.
Awali August 23 na 24 mwaka huu Mwenyekiti wa
Kijiji cha Lugarawa Bw. Erasto Mhagama akiwa na Mwenyekiti wa Kitongoji cha
Luafyo Juu walikwenda kumpigia magoti Padri Jordan Mwajombe ili afute msimamo
wake na badala yake atoe maji kwa wananchi, lakini alikataa kabisa na kuwafokea
kama watoto wadogo viongozi hao.
Mwenyekiti wa Kitongoji cha Luafyo Juu Mzee Thadei
Exavery Mwinuka (70) kwa upande wake alisema anayo miaka zaidi ya thelathini
katika eneo hilo na muda wote wananchi wake wamekuwa wakitumia maji hayo
yaliyoletwa kwa ushikiano wa wenyeji na wamisionari wazungu.
Mzee Mwinuka alisema sababu za wananchi
kukata mabomba haya ni kunatokana na ukatili wa ...