Skip to main content

Posts

Showing posts from September 4, 2011

WANANCHI WENYE HASIRA LUGARAWA WAKATA MABOMBA YA MAJI YA PAROKO, NI BAADA YA MWENYEKITI WAO KUMPIGIA MAGOTI BILA MAFANIKIO.

LUDEWA WANANCHI na watumiaji wa maji katika Kitongoji cha Luafyo Juu Lugarawa wilayani Ludewa jana walijawa jazba na kuamua kuyakata kwa mapanga mabomba ya maji yanayotumika pia na Kanisa Katoliki kwa madai kuwa Paroko wao amewanyima maji bila sababu. Awali August 23 na 24 mwaka huu Mwenyekiti wa Kijiji cha Lugarawa Bw. Erasto Mhagama akiwa na Mwenyekiti wa Kitongoji cha Luafyo Juu walikwenda kumpigia magoti Padri Jordan Mwajombe ili afute msimamo wake na badala yake atoe maji kwa wananchi, lakini alikataa kabisa na kuwafokea kama watoto wadogo viongozi hao. Mwenyekiti wa Kitongoji cha Luafyo Juu Mzee Thadei Exavery Mwinuka (70) kwa upande wake alisema anayo miaka zaidi ya thelathini katika eneo hilo na muda wote wananchi wake wamekuwa wakitumia maji hayo yaliyoletwa kwa ushikiano wa wenyeji na wamisionari wazungu. Mzee Mwinuka alisema sababu za wananchi kukata mabomba haya ni kunatokana na ukatili wa ...