Skip to main content

Posts

Showing posts from April 16, 2018

LIPULI FC YATAMBA KUICHAPA SIMBA SC

Wachezaji wa wakigombania mpira wa kona katika lango la timu ya Lipuli wakati wa mechi dhidi ya Singida United (jezi la rangi ya kijani) ya mkoani Singida katika Uwanja wa CCM Samora mjini Iringa Jumapili. Timu ya Lipuli ilishinda 1-0. (Picha na Friday Simbaya) Mshambuliaji wa Timu ya Singida United Deus Kaseke mwenye jezi namba saba (7) mgongoni akijaribu kumtoroka Beki wa timu ya Lipuli FC Daruwesh Saliboko katika mechi iliyopigwa Jumapili katika Uwanja wa CCM Samora mjini Iringa. Lipuli FC iliishinda Singida United 1-0. (Picha na Friday Simbaya) Mshambuliaji machachari wa Timu ya Lipuli ya mjini Iringa Malimi Busungu akishangilia baada ya kufunga bao la kwanza ndani ya dakika 17 kipindi cha kwanza ya mechi dhidi ya Singida United jana (Jumapili) katika uwanja wa CCM Samora mjini Iringa. Matokeo mechi hiyo Lipuli FC dhidi ya Singida United yalikuwa 1-0. (Picha na Friday Simbaya) Mashabiki wa Timu ya Lipuli FC wakisangilia timu ya kwa mavuvuzela dhidi ya Sin...