Skip to main content

Posts

Showing posts from January 16, 2016

Msichana aongoza Form II kitaifa

Katibu Mtendaji wa Baraza hilo, Dk. Charles Msonde. Baraza la Taifa la Mitihani (NECTA), limetangaza matokeo ya kidato cha pili huku msichana, Lineth Christopher kutoka Shule ya Sekondari ya St. Aloysius Girl’s ya mkoani Pwani, aking’ara kitaifa. Matokeo hayo yalitangazwa jana jijini Dar es Salaam na Katibu Mtendaji wa Baraza hilo, Dk. Charles Msonde, ambaye alisema waliofanya mtihani huo mwaka jana walikuwa ni wanafunzi 363,666 sawa na asilimia 91.66. Alisema kati ya walioufanya mtihani huo, waliofaulu ni wanafunzi 324,068 sawa na asilimia 89.12, ambapo wasichana ni 164,547 sawa na asilimia 89.00 na wavulana ni 159.521 sawa na asilimia 89.24. Dk. Msonde alisema wanafunzi 39,567 sawa na asilimia 10.88 walishindwa kupata alama za kuwawezesha kuendelea na masomo ya Kidato cha tatu; hivyo watarudia darasa wakati wanafunzi 33,104 sawa na asilimia 8.34 hawakufanya mtihani huo kwa sababu za utoro na magonjwa. Alisema idadi ya watahiniwa waliopata ufaulu mzuri wa mad...

Serikali ya JK ilipoteza trilioni 30/- miaka mitano.

Rais John Magufuli Kuongezeka kwa makusanyo ya kodi katika serikali ya Rais John Magufuli hadi kufikia Sh.trilioni 1.4 kwa mwezi, kunadhihirisha kwamba kulikuwapo na upotevu wa mapato ya Sh.trilioni 30 kwa kipindi cha miaka mitano ya mwisho ya Rais wa nne, Jakaya Kikwete. Serilali ya JK ilikuwa ikikusanya wastani wa Sh. bilioni 900 kwa mwezi. Kuwapo kwa utofauti ya wastani wa Sh.bilioni 500 kwa mwezi wa makusanyo ya kodi baina ya serikali ya Magufuli na ya Kikwete, inaonyesha kulikuwapo na mianya mingi ya uvujaji wa mapato kwa miaka mitano ya mwisho ya uongozi wake kuliko tu wizi wa makontena katika Bandari ya Dar es Salaam. Kaimu Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Alphayo Kidata, aliwaambia waandishi wa habari Januari 4 kuwa wamevuka lengo la makusanyo ya mwezi Desemba; baada ya kukusanya Sh. trilioni 1.4, ikiwa ni ongezeko la wastani wa Sh.bilioni 500 kwa mwezi. Kwa kipindi cha miaka mitano ambayo ni sawa na miezi 60 ya uongozi wa Rais Kikwet...

Mwalimu akutwa amejinyonga chumbani

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Revocatus Malimi. NA WAANDISHI WETU Mwalimu wa Shule ya Msingi Peramiho, Songea mkoani Ruvuma, Baraka Mwakajila (29), amekutwa amefariki dunia baada ya kujinyonga kwa kutumia shati ndani ya nyumba alimokuwa akiishi. Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Revocatus Malimi, alisema jana kuwa tukio hilo limetokea juzi saa sita mchana katika mji mdogo wa Peramiho, nje kidogo ya Manispaa ya Songea. Malimi alisema inadaiwa kuwa siku hiyo ya tukio, Mwalimu Mkuu Msaidizi, Rashid Pilly, aligundua kujinyonga kwa mwalimu huyo, baada ya kupita eneo la nyumba aliyokuwa anaishi na kuona nzi wengi wametapakaa kwenye eneo la dirisha la chumba alichokuwa analala. Alifafanua zaidi kuwa Mwalimu Pilly baada ya kuona hali hiyo, alisogea hadi mlangoni na kukutwa mlango ukiwa umefungwa huku eneo hilo likiwa na harufu kali iliyoashiria kuna kitu ambacho kimeoza. Alisema baadaye Mwalimu Pilly alilazimika kwenda kutoa taarifa kwenye ...

Burkina Faso security frees 120 hostages in AL-Qaeda hotel attack

Assault begins at second hotel in capital of Ouagadougou after up to 20 killed in hotel popular with UN staff and foreigners Fire and smoke rising from the Splendid hotel in Ouagadougou where militants are holding hostages. Photograph: Reuters Nadia Khomami and agencies in Ouagadougou Burkina Faso security forces have freed more than 120 hostages from a hotel seized by al-Qaida-linked fighters in the capital of Ouagadougou, but a second assault has begun at another hotel nearby, according to reports. “Three jihadists were killed. They were an Arab and two black Africans,” Simon Compaore, the country’s security minister, said of the raid which concluded early on Saturday morning. Up to 20 people had been killed and 33 people wounded in the attack, with forces still determining the number of casualties. Islamic extremists invaded the Splendid hotel and the Cappuccino cafe on Friday night. The militants took control of the five-storey hotel, which is popular w...

TASWIRA MBOVU YA BARABARA YA "MARKET STREET" JIJINI MWANZA

Hii ni barabara inayotegemewa na daladala za Bwiru-Kisesa, Airtport- Kishiri pamoja na Ilemela-Kishiri hii ikiwa ni kwa upande wa daladala. Lakini pia ikitegemewa na watumiaji wengine wa vyombo vya moto vya binafsi. Ni barabara iliyotumika pia na wakazi wengi wa Jiji la Mwanza wakiwa wanatoka katika mizunguko yako ikiwemo kutoka Soko Kuu la Jiji la Mwanza. Kama inavyoonekana katika picha inahitaji msaada maana wakati huu wa mvua imeharibika sana. "Hii barabara inaharibika mara kwa mara kutokana na mitaro iliyopo hapa kuziba mara kwa mara kutokana na wafanyabiashara katika maeneo haya kuwa na tabia ya kutupa makopo mitaroni na hivyo kusababisha mitaro kuziba na hivyo mvua ikinyesha maji yanajaa katika barabara hii na hatimae kusababisha hali hii unayoiona". Binagi Media Group imeeleezwa na baadhi ya wafanyabiashara waliopo jirani na barabara hiyo. Watumiaji wa barabara hiyo wameiomba halmashauri ya Jiji la Mwanza pamoja na Mbunge wa Jimbo la Nyamagana kushu...

KESI YA KUPINGA MATOKEO JIMBO LA BUNDA MJINI YAAHILISHWA

Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza leo imeanza kusikiliza Kesi ya Kupinga Matokeo ya uchaguzi Mkuu uliofanyika Novemba 25 mwaka jana katika Jimbo la Bunda Mjini, Mkoani Mara ambapo Mgombea kutoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Esther Bulaya aliibuka mshindi. Na:George Binagi-GB Pazzo Jaji wa Mahakama hiyo Mhe.Mohamed Gwae ameahirisha kesi hiyo hadi jumatatu ijayo ya Januari 25 mwaka huu baada ya mawakili wa pande zote mbili kuchuana vikali kwa muda mrefu.  Waleta maombi (Mlalamikaji) katika kesi hiyo wametajwa kuwa ni wapiga kura wa jimbo hilo la Bunda Mjini ambao walikuwa wakiiomba Mahakama kutengua matokeo ya uchaguzi huo katika jimbo hilo kutokana na uchaguzi huo kukumbwa na kasoro mbalimbali ikiwemo uchaguzi kutokuwa huru pamoja na idadi ya wapiga kura kutofautiana na idadi ya waliojiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura. Madai hayo yamepingwa na upande wa Mjibu Maombi (Walalamikiwa ambao ni Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini pamoja na Mwa...

TIGO YAFUNGUA DUKA LA KISASA SAME

Katibu wa wilaya ya Same Mhe. Evagry Keiya (katikati)akikata utepe kufungua duka la Tigo Same, wanaoshuhudia ni Meneja wa huduma kwa wateja Tigo, Mwangaza Matotola(kushoto) na Mkurugenzi wa Tigo kanda ya Kaskazini George Lugata(kulia) mapema mwishoni wa wiki iliyopita  Baadhi ya wafanyakazi wa Tigo wakiwa katika tafrija ya ufunguzi wa duka la Tigo Same mapema wa mwishoni wa wiki iliyopita  Mkurungezi wa Tigo kanda ya kaskazini Bw.George Lugata akitoa hotuba wakati wa ufunguzi wa duka la Tigo Same mapema mwishoni wa wiki iliyopita  Baadhi ya wageni waalikwa wakiwa kwenye tafrija ya kufungua duka la Tigo same wakisikiliza kwa makini hotuba ya mgeni rasmi Mh Evagry Keiya mapema mwishoni wa wiki iliyopita  Kampuni  ya simu ya Tigo imefungua duka jipya la same ambalo limepunguza adha kwa wateja wa  kampuni hii ambao walikuwa wanatafuta huduma kwa wateja umbali mrefu toka kwa makazi yao  Akizu...