Skip to main content

Posts

Showing posts from September 21, 2017

SHAHIDI AIELEZA MAHAKAMA JINSI DC ALIVYOPEKUWA CHUMBA CHAKE

Na Woinde Shizza SHAHIDI wa utetezi katika kesi ya kughushi Mukhtasari,wa serikali ya mtaa wa Levolosi ,mfanyabiashara ,Mathew Moleli ameieleza mahakama jinsi mkuu wa wilaya mstaafu alivyoingia kwa mabavu nyumbani kwake na kuamrisha askari polisi aliokuwa ameambatana nao wapekuwe chumba chake wakitafuta hati inayodaiwa kughushiwa. Akitoa utetezi mbele ya hakimu Gwanta Mwankuga wa mahakama ya hakimu mkazi Arusha ,anayesikiliza shauri hilo huku akiongozwa na wakili wa utetezi Ephraim Koisenge, aliieleza mahakama hiyo jinsi alivyofedheheshwa wakati askari hao,akiwemo mwendesha bodaboda na mlalamikaji Makanga walivyopekuwa chumba chake wakitafuta hati ambayo ni mali. Shahidi huyo aliiendelea kueleza kuwa, mnamo oktoba ,2 mwaka 2014 alishtakiwa katika mahakama ya wilaya iliyopo Sekei mkoani Arusha, kwa shauri kama hilo huku mlalamikaji akiwa ni Danny Makanga na baadae oktoba 1,mwaka 2015 kesi hiyo ilifutwa baada ya upande wa jamhuri kuomba kuondoa shauri hilo mahakam...

AVUNJWA MGUU KWA RISASI

Mkazi wa kitongoji cha Endevesi ,kata ya Oljoro wilaya ya Arumeru,Hwanga Ndaskoy(30)amefunjika mkuu wake wa kulia baada ya watu wanaodaiwa kuwa ni askari polisi mkoani Arusha, wapatao nane kumvamia na kumpigwa risasi ,akiwa shambani kwake . Akizungumza kwa masikitiko nyumbani kwake, baada ya kuruhusiwa kutoka hospitali ya Mount Meru alikokuwa amelazwa kwa zaidi ya wiki moja,Ndaskoy ameeleza kwamba tukio hilo limetokea mnamo,Agost 31,mwaka huu majira ya saa saba wakati akivuna mahindi shambani kwake akiwa na familia yake. Alisema kua alifuatwa na askari hao waliokuwa wamevalia kiraia na mmoja mwenye silaha akiwa amevaa sare za kipolisi. Pia askari hao walikuwa wameongozana na mkazi mmoja wa kitongoji hicho aliyemtaja kwa jina la ,Yohane Palay aliyemtambua kuwa ni baba mkwe wake . ‘’Nilimsikia baba mkwe akiwaelekeza askari hao wanikamate huku akiwatahadhalisha kuwa mimi ni mkorofi na wasinisogelee nitawakata na sime jambo ambalo sio kweli,ndipo askari mmoja...