Skip to main content

Posts

Showing posts from March 18, 2026

Lori la Tanzania Lapinduka Karibu na Tenke Fungurume, DRC

Lori lenye namba za usajili wa Tanzania, linalodaiwa kubeba shehena ya Copper Cathodes , limepinduka karibu na eneo la mgodi wa Tenke Fungurume Mining katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC). Taarifa za awali zinaeleza kuwa chanzo cha ajali hiyo bado hakijafahamika. Hata hivyo, barabara ya mteremko kutoka Kolwezi kuelekea Fungurume inatajwa kuwa hatari na yenye changamoto kubwa kwa magari mazito, hali inayoweza kuwa sababu ya ajali hiyo. Kwa sasa, eneo la tukio linalindwa na askari wenye silaha kutoka vyombo vya usalama vya DRC, wakiwemo polisi na wanajeshi, ili kuhakikisha usalama wa mzigo uliokuwamo kwenye lori hilo. Hadi kufikia sasa, hali ya dereva wa lori hilo bado haijathibitishwa. Taarifa zaidi zitaendelea kutolewa kadri zitakavyopatikana. Wananchi wametakiwa kuendelea kuchukua tahadhari wanapotumia barabara, hasa katika maeneo yenye miinuko mikali.  

Mahakama Kuu Yamuhukumu Kifo Baba Aliyemuua Mtoto Wake kwa Imani za Utajiri

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Iringa imemhukumu kunyongwa hadi kufa, Joseph Muhulila (28), mkazi wa Mtaa wa Lukosi, Kata ya Mkwawa, Manispaa ya Iringa, baada ya kupatikana na hatia ya kumuua kwa makusudi mtoto wake wa kumzaa, Timothy Muhulila (miaka 4), akidaiwa kufanya hivyo kwa imani za kujipatia utajiri. Hukumu hiyo iliyosomwa kwa zaidi ya saa nne imetolewa na Jaji Angaza Mwipopo katika kesi namba 25532 ya mwaka 2025, akieleza kuwa ushahidi uliowasilishwa mahakamani umethibitisha bila kuacha shaka kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo kinyume cha vifungu vya 196 na 197 vya Sheria ya Kanuni ya Adhabu, Sura ya 16 ya mwaka 2022. Upande wa Jamhuri uliwakilishwa na mawakili David Mwakiborwa na Jackson Mwakalinga. Kwa mujibu wa mahakama, tukio hilo la kikatili lilitokea Aprili 12, 2025, ambapo mshtakiwa alimuua mtoto wake kisha kumkatakata vipande vidogo na kuvitupa kwenye shimo la choo. Akisoma maelezo ya ushahidi, Jaji Mwipopo alinukuliwa akisema: “Mtuhumiwa alikiri kukata mwili wa marehe...