Skip to main content

Posts

Showing posts from October 26, 2025

ASAS AWATOA HOFU WANANCHI KUHUSU VURUGU ZA UCHAGUZI

MJUMBE wa Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Salim Abri Asas , amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, huku akiwatoa hofu juu ya uvumi unaoenezwa mitandaoni kuhusu uwepo wa vurugu siku ya uchaguzi huo. Asas amesema kumekuwepo na taarifa zisizo sahihi kutoka kwa baadhi ya watu, ndani na nje ya nchi, wanaotumia mitandao ya kijamii kuhamasisha maandamano na kuchochea vurugu ambazo zinaweza kuhatarisha amani na kuathiri zoezi la uchaguzi. Akihutubia maelfu ya wanachama na wananchi katika mkutano wa kufunga kampeni za CCM Jimbo la Mafinga Mjini, uliofanyika katika kijiji cha Ugute, kata ya Isalavanu, Halmashauri ya Mji Mafinga, Asas aliwahakikishia wananchi kuwa nchi ipo salama na vyombo vya ulinzi na usalama vimejipanga kikamilifu kulinda amani. “Nataraji katika siku hizi mbili mtajitokeza kwa wingi kupiga kura siku ya Oktoba 29. Msiogope wala kuwa na hofu, amani ipo na kutakuwa na ulinzi wa kutosha. Nchi yetu imetulia — hayo yote ...