Skip to main content

Posts

Showing posts from November 23, 2011

KIKWETE AKATA MZIZI WA FITINA KUHUSU GARI LA WAGONJWA MLANGALI AWALI WANANCHI WALIJIPANGA BARABARANI KUKUMBUSHA AHADI YA RAIS, MADIWANI WAPIGWA MSHANGAO

Ludewa RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Jakaya Mrisho Kikwete jana alikata mzizi wa fitina kutokana na utata uliokuwepo kati ya wananchi na Baraza la Madiwani kuhusu gari la wagonjwa   Namba SM 9192 aliloahidi kwa Kituo cha Afya Mlangali mwaka 2008. Dr. Kikwete alifikia hatua hiyo baada ya wananchi wa Kata ya Mlangali waliokuwa wamesimama barabarani kumlaki na alipowataka watoe shida zao wakamwambia kuwa wanashukuru kwa kutimiza ahadi ingawa wameipata jana wakati gari hilo lina zaidi ya miezi saba wilayani. Wananchi wa Mlangali pamoja na mambo mengine walimwambia Rais kuwa katika Kata yao wanakabiliwa na mambo mengi ikiwemo maji safi, barabara, gari la kubebea wagonjwa (Ambulance) na umeme. Madiwani katika kikao chao cha Julai 15 mwaka huu walikubaliana kwa kauli moja kuchukua gari la kubebea wagonjwa (Ambullance) No. SM 4677 lililokuwa katika Hospitali ya Wilaya na kulipeleka Lupingu ili kuwahudumia wananchi wa Mwambao na gari SM 9192 lililotolewa ...

DC LUDEWA, SITAYUMBISHWA NA WAWEKEZAJI WATAKAOVUNJA SHERIA ZA NCHI MCHUCHUMA NA LIGANGA.

Ludewa MKUU wa Wilaya ya Ludewa mkoani Iringa Bi Georgina Bundala amekana kutoyumbishwa kwa namna yoyote ile na wawekezaji wataovunja sheria za nchi na zile zilizopo katika mikataba ya sheria ya madini ya Liganga na Mchuchuma. Bi Georgina aliwaambia waandishi wa habari jana ofisini kwake ambao pamoja na mambo mengine walitaka kujua amejipanga vipi na nini msimamo wake kwa wawekezaji wenye tabia ya kuwayumbisha viongozi, hasa wakuu wa wilaya nchini waliopo ndani ya migodi kwa manufaa yao binafsi. Aliongeza kuwa wawekezaji wengi nchini wanapokuja kuomba kuwekeza wanakuwa na nidhamu na kuonesha ushirikiano wenye kuleta ufanisi kwa nia nzuri ya kuchochea chachu ya kuwaletea maendeleo wananchi waishio maeneo ya migodi, lakini baadaye hugeuka na kuwafanya wananchi kuwa wakimbizi nchini mwao siko tayari kuwaonea aibu, alisisitiza. “Sheria za nchi zipo wala sina haja ya kuumiza kichwa na kupoteza muda mtu yeyote atakayekiuka au kuvunja sheria kwa lengo la kuwanyanyasa ...

LHRC, YAAMSHA MADIWANI LUDEWA, NI KUHUSU HAKI ZA BINADAMU NA WAJIBU ZAO.

Ludewa   HUKU Tanzania ikiadhimisha miaka Hamsini ya Uhuru madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa katika Mkoa Iringa bado wanabanwa na mfumo wa utawala na kushindwa kusimamia mali za umma. Wakizungumza jana katika semina ya siku tatu kuhusu sheria za kazi, rushwa na utawala bora, haki za binadamu, Katiba, wajibu na maadili ya diwani, iliyoendeshwa na Kituo Cha Sheria na Haki za Binadamu walipongeza kituo hicho kwa kuwafumbua macho. Madiwani hao walilalamikia mifumo na miongozo mibaya ya TAMISEMI inayoleta urasimu kwa nia ya kudhoofisha nafasi na hadhi ya madiwani kwa wananchi jambo linalopelekea kudharauliwa na watumishi wa Halmashauri. Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa Bw. Emanuel Mlelwa ambaye ndiye alikuwa mgeni rasmi katika ufunguzi wa mafunzo hayo alisema mafunzo haya yamekuja wakati mwafaka kwa madiwani hao kutokana na wengi wao kutokujua vyema sheria, maadili na wajibu zao. Mlelwa aliwataka madiwani kuwa wasikivu kwani mafunzo h...