Skip to main content

Posts

Showing posts from January 31, 2018

IMC Yasaini Mkataba Wa 3.7bn/- Kwa Ajili Ya Ujenzi Wa Soko La Kisasa La Mlandege

mwakilishi wa Kampuni iliyoshinda zabuni hiyo Home Africa Investment Corporation ya jijini Dar es salaam  Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa Ndugu, Omary Mkangama, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Iringa Mheshimiwa Alex Kimbe, Halmashauri ya Manispaa ya Iringa imesaini mkataba wa ujenzi wa soko la kisasa katika Kata ya Mlandege wenye thamani ya shilingi Bilioni 3,725,236,998/= chini mradi wa kusaidia uendelezaji wa mji( Urban Local Government Support Programme unaofadhiliwa na Benki ya Dunia.  Mkataba huo umesainiwa na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Iringa Mheshimiwa Alex Kimbe, Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa, Omary Mkangama, mwakilishi wa Kampuni iliyoshinda zabuni hiyo Home Africa Investment Corporation ya jijini Dar es salaam chini ya usimamizi wa Mwanasheria wa Manispaa ya Iringa Ndugu, Charles P. Lawisso , wakuu wa Idara na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali.  Halmashauri ya Manispaa ya Iringa ni miongoni mwa Mamlaka za Serikali za Mitaa( M...

AZAM YAIPA MCHECHETO SIMBA,SIMBA YAAMUA KUIANGUKIA BODI YA LIGI

Vinara wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Simba ni kama imeanza kuingia mchecheto baada ya kuitaka Bodi ya Ligi (TPLB) kusogeza mbele mechi yake dhidi ya Azam iliyopangwa kuchezwe Februari 11 mwaka huu. Simba yenye pointi 35, inachuana vikali na Azam wenye 30 katika msimamo wa ligi na Mabingwa watetezi Yanga waliovuna 28, katika kuliwania taji hilo la ubingwa la ligi. Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa timu hiyo, Haji Manara alisema ratiba yao inawapa ugumu kutokana na akili na nguvu zao kuzielekeza kwenye michuano ya kimataifa na Simba imepangwa kucheza Gendarmerie Nationale ya Djibouti kati ya Februari 9-11, mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Manara alisema, ratiba hiyo inawapa ugumu kwani Simba itacheza na Ruvu Shooting Februari 4 na kucheza na Azam kabla ya kwenda Shinyanga kucheza na Mwadui huku wakiusubiria mchezo wao wa kimataifa. “Mipango ya Simba ni kufika mbali katika michuano ya Afrika na hiyo ndiyo sababu ya sisi...