SONGEA Mratibu wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS) Mkoa wa Ruvuma Bwana Emmanuel Petro amesema kuwa ili kupunguza kasi ya maambukizo ya Virusi Vya Ukimwi mkoani hapa halmashauri na wadau wengine wa Ukimwi hazina budi kufanya kazi kwa pamoja. Alisema kuwa ili kufanikisha mkakati wa taifa wa kinga dhidi ya VVU halmashauri na wadau wengine wanapaswa kufanya kazi kwa karibu na hatimaye kuweza kupunguza maambukizo haya. Mratibu TACAIDS (M) huyo alitoa rai jana katika kikao cha kupitia mipango ya shughuli za Ukimwi za Halmashauri kilichofanyika Peramiho kikihusisha Waratibu wa Ukimwi Kinga Wilaya (CHAC) na Waratibu wa Ukimwi-Tiba katika ngazi ya wilaya yaani (DACC) wa kutoka Halmashauri zote za Wilaya zote za Mkoa wa Ruvuma yaani Songea Manispaa, Songea Vijijini, Namtumbo, Mbinga na Tunduru. Alisema kuwa lengo la kikao hicho cha siku mbili ni kupima shughuli za Ukimwi za halmashauri kama zinaendana na miongozo ya kitaifa,kama ...
Pamlomo-Sauti Ya Jamii (SYJ) is essentially a digital news platform that shares different types of news updates — social, political, economic, sports, entertainment, and community stories. From the context you’ve given, it is based in Iringa, Tanzania, and functions mainly as an online outlet (likely through social media such as Facebook, YouTube, or other channels) where audiences can get real-time updates.