Skip to main content

Posts

Showing posts from March 9, 2026

WANAWAKE WA TFS SAO HILL WAWAFARIJI WATOTO YATIMA MUFINDI

Mhifadhi Mkuu wa Shamba la Miti Sao Hill, PCO Tebby Yoramu akiwa anamfariji mtoto wa y atima wa kituo cha Caring from Childhood to Youth kilichopo katika kijiji cha Bumilayinga,wakati wa  kilele cha maadhimisho ya  Siku ya Wanawake Duniani , Mhifadhi Mkuu wa Shamba la Miti Sao Hill,  PCO Tebby Yoramu akiwa akikabidhi zawadi   katika  kituo cha watoto yatima cha Caring from Childhood to Youth kilichopo katika kijiji cha Bumilayinga,wakati wa  kilele cha maadhimisho ya  Siku ya Wanawake Na Fredy Mgunda, Mufindi Wanawake wahifadhi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kutoka Shamba la Miti Sao Hill wametembelea na kuwafariji watoto wanaolelewa katika Kituo cha Kulelea Watoto Yatima cha Caring from Childhood to Youth kilichopo katika kijiji cha Bumilayinga, wilayani Mufindi mkoani Iringa. Ziara hiyo imefanyika ikiwa ni sehemu ya shughuli za kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, ambapo wanawake hao walionyesha upendo na m...

Dkt. Tulia Akabidhi Nyumba kwa Familia ya Mzee Tuli Mwantindili

Na Hawa Matias, Mbeya Mbeya, Machi 07, 2026 – Taasisi ya Tulia Trust, chini ya uongozi wa Dkt. Tulia Ackson, Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Mbunge wa Jimbo la Uyole, imemkabidhi nyumba ya kuishi familia ya Mzee Tuli Mwalwala Mwantindili. Nyumba hiyo, iliyojengwa kupitia mpango wa Tulia Trust – Mtaani Kwetu, ni nyumba ya 23 kwa ajili ya watu wenye uhitaji. Kwa nyumba hizo, nne (4) zimejengwa nje ya Jiji la Mbeya. Familia ya Mzee Mwantindili inayoishi mtaa wa Itongo, Kata ya Mwakibete, imepata makazi mapya leo. Akizungumza katika hafla ya makabidhiano, Dkt. Tulia aliwaasa wananchi wa kata hiyo kuendeleza utamaduni wa kusaidiana na kushirikiana katika changamoto mbalimbali zinazowakabili baadhi ya wananchi. "Sisi kama jamii tuendelee kushirikiana na kusaidiana kwenye changamoto mbalimbali tulizonazo hata kwa kidogo tulichonacho," alisema Dkt. Tulia. Aidha, Dkt. Tulia ametoa iftari kwa waumini 1,000 wa dini ya Kiislam katika hafla fupi iliyoandaliwa nyumbani ...

Tanzania celebrates Commonwealth Day

  Iringa. Tanzania has joined other member states of the Commonwealth of Nations in marking Commonwealth Day today, March 9, 2026, with cultural activities, school events and faith-based services. Observed annually on the second Monday of March since 1977, the day brings together people from across the Commonwealth—representing nearly a third of the world’s population—in a shared moment of reflection and celebration. This year’s theme, “Unlocking opportunities together for a prosperous Commonwealth,” highlights how countries and communities can collaborate to improve people’s lives, including creating decent jobs and expanding access to quality education. Celebrations are taking place in many forms across the world. From Samoa to Saint Lucia, and among diaspora communities globally, people are marking the day through activities rooted in local traditions, including memorial services, festivals and street parades. In Antigua and Barbuda, the occasion is being marked by cultu...

Mtoto (13) Afariki Dunia Akidaiwa Kufanyiwa Ukatili Wa Kingono Iringa

Iringa. Mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 13, mkazi wa Mtaa wa Njiapanda, Kata ya Isakalilo katika Manispaa ya Iringa, amefariki dunia baada ya kudaiwa kufanyiwa ukatili wa kingono. Mtoto huyo ambaye alikuwa mwanafunzi wa darasa la saba katika Shule ya Msingi Zizi, alikutwa akiwa amefariki nje ya nyumba yao, tukio lililosababisha taharuki na huzuni kwa wakazi wa eneo hilo. Kwa mujibu wa majirani na ndugu wa familia, mwili wa mtoto huyo uligunduliwa asubuhi ya Machi 7, 2026, nje ya nyumba yao baada ya juhudi za kumtafuta kuanza kufanyika kufuatia kutoweka tangu usiku. Jirani wa familia hiyo, Jacob Mwalongo, alisema walifanya jitihada za kumtafuta mtoto huyo bila mafanikio, kabla ya kutoa taarifa katika kituo cha polisi. “Tulianza kumtafuta huku na kule lakini hatukumpata. Jioni tulikwenda kutoa taarifa polisi. Asubuhi tulipata taarifa kutoka kwa jirani mmoja kuwa mtoto amepatikana akiwa ameanguka karibu na nyumba. Tulipofika eneo hilo tulikuta tayari amefariki dunia ndipo tukar...