Skip to main content

Posts

Showing posts from April 18, 2026

FESTO KISWAGA ACHUKUA NA KUREJESHA FOMU KUWANIA UBUNGE ISIMANI

  Aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Monduli, Festo Kiswaga, amechukua na kurejesha rasmi fomu ya kuomba ridhaa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kugombea ubunge wa Jimbo la Isimani, mkoani Iringa.  Zoezi hilo limefanyika katika ofisi za CCM Wilaya ya Iringa Vijijini, ikiwa ni sehemu ya mchakato wa ndani wa chama hicho kuelekea uchaguzi mdogo wa jimbo hilo.  Kiswaga, aliyewahi kushika nyadhifa mbalimbali za uongozi serikalini, ni miongoni mwa wanaowania nafasi hiyo ya ubunge, akilenga kurithi kiti kilichoachwa wazi kufuatia kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Isimani, William Lukuvi, ambaye pia aliwahi kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Ajira na Wenye Ulemavu).