Skip to main content

Posts

Showing posts from September 8, 2016

KUMEKUCHA DODOMA,TIZAMA MAKAZI YA WAZIRI MKUU DODOMA

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary (kulia kwake ) wakikagua ujenzi wa makazi mapya ya Waziri Mkuu kwenye kilima cha Mlimwa mjini Dodoma Septemba 7, 2016. Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Badhi ya Mawaziri na viongozi wa mkoa wa Dodoma baada ya kukagua ujenzi wa makazi mapya ya Waziri Mkuu kwenye kilima cha Mlimwa mjini Dodoma Septemba 7, 2016. Katikati ni mkewe Mary.  (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) SERIKALI YAPITISHA MISWAADA HII KUWA SHERIA Na Eleuteri Mangi-Maelezo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ameridhia na kusaini Miswada mitano kutumika kama Sheria kamili za nchi. Hayo yamesemwa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai mara baada ya kufungua Mkutano wa nne wa Bunge la 11 leo mjini Dodoma. Miswada iliyoidhinishwa na Rais ni pamoja Sheria ya Fedha na Matumizi ya mwaka 2016, Sheria ya Fedha namba 2 ya mwaka 2016, Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali...

MKURUGENZI MTENDAJI MPYA WA TACAIDS AJITAMBULISHA KWA WADAU WA UKIMWI

Mkurugenzi Mtendaji wa Tacaids, Dk. Leonard Maboko. Mkurugenzi Mtendaji Mpya wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS), Dk. Leonard Maboko (kushoto), akizungumza na wadau wa ukimwi katika mkutano wa kufahamiana uliofanyika Makao Makuu ya Tacaids Dar es Salaam leo. Kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Sheria (Tacaids), Elizabeth Kaganda na Mkurugenzi wa Ufatiliaji na Tathmini, Dk. Jerome Kamwela. Wadau wa ukimwi wakimsikiliza mkurugenzi wao mpya. Wadau wa ukimwi wakimsikiliza mkurugenzi wao. Mkurugenzi wa wa Habari na Uraghibishi, Jumanne Isango na Mkurugenzi wa Utawala na Fedha wa Tacaids, Yasin Abbas wakiwa kwenye mkutano huo.  Taswira ya mkutano huo.