Skip to main content

Posts

Showing posts from January 19, 2017

SERIKALI YAONYA WAWEKEZAJI WANAOCHOCHEA MIGOGORO

Na Woinde Shizza,Arusha.  Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amesema kuwa serikali haitasita  kuwachukulia hatua wawekezaji wanaochochea migogoro katika wilaya ya  Ngorongoro na kusababisha uvunjifu wa amani hivyo kuchangia kuzorota kwa  shughuli za maendeleo.  Gambo ameyasema hayo katika ziara yake wilayani Ngorongoro inayolenga  kutatua migogoro wa pori tengefu lenye ukumbwa wa kilomita za mraba elfu  kumi na tano ambapo amekutana na wadau mbalimbali ikiwemo  wawekezaji,wafugaji pamoja na viongozi wa kiserikali.  Amesema kuwa serikali itawaondoa wawekezaji wanaochochea migogoro na  kuwagombanisha wananchi na serikali yao jambo ambalo halitafumbiwa  macho  Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro Rashid Taka amesema kuwa wako baadhi ya watu  wanaonufaika na migogoro hiyo hivyo kumalizika kwa migogoro hiyo kutaleta  manufaa kwa wananchi wengi kuliko kunufaisha kundi la watu  wachache...