Skip to main content

Posts

Showing posts from November 24, 2016

RAIS MAGUFULI NA RAIS MSTAAFU MWINYI WAKUTANA IKULU

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe 23 Novemba, 2016 amekutana na kufanya Mazungumzo na Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Alhaji Dkt. Ali Hassan Mwinyi, Ikulu Jijini Dar es Salaam. Baada ya mazungumzo hayo, Alhaji Dkt. Ali Hassan Mwinyi amesema lengo la kukutana na Rais Magufuli na kufanya nae mazungumzo kwa mara ya kwanza ni kumpongeza kwa kutimiza mwaka mmoja tangu aingie madarakani na pia kumpongeza kwa kazi kubwa aliyoifanya katika kipindi kifupi cha uongozi wake. Alhaji Dkt. Ali Hassan Mwinyi ameyataja baadhi ya maeneo ambayo Rais Magufuli ameyafanya kwa mafanikio makubwa kuwa ni mapambano dhidi ya rushwa na amebainisha kuwa hatua zilizochukuliwa katika kipindi cha mwaka mmoja zimedhihirisha kasi kubwa ya kukabiliana na tatizo hilo ikilinganishwa na wakati uliopita. “Rushwa ilikuwepo tangu enzi ya Hayati Mwalimu Nyerere, aliipondaponda kabisa lakini hakuimaliza, na sote tuliosalia ni hivyo hivyo, kila mmoja amefanya kwa ...

WAZIRI MWAKYEMBE AJIPANGA KUWAFUKUZA MAHAKIMU WENYE CHETI NA DIPLOMA

Waziri wa katiba na sheria Mh. Dkt Harrison Mwakyembe amesema serikali itawafuta kazi mahakimu wote wa mahakama ya mwanzo wenye elimu ya cheti na diploma ya sheria. “Tunahitaji mahakimu wenye uwezo wa sheria ambao wamehitimu shahada ya kwanza,hivyo serikali itawafuta kazi mahakimu wote wenye elimu ya cheti na diploma”  Dkt Mwakyembe ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mswada wa sheria ya msaada wa kisheria ambapo amewaomba wananchi na wadau wa sheria nchini kufanyia mapitio mswada huo na kutoa maoni yao kwa kamati ya bunge ya katiba na sheria wakati utakapowadia. Dkt Mwakyembe amesema bunge litaweka utaratibu unaofaa kwa ajili ya kupokea maoni ya wadau wote watakaofika mbele ya kamati na wale watakao wasilisha maoni yao kwa njia ya maandishi. Aidha waziri mwakyembe ameelezea mswada huo ambao umesomwa bungeni kwa mara ya kwanza tarehe 10 novemba utawatambua watoa huduma za msaada wa kisheria na utakuwa ni ...

WASHINDI WA SINGELI IRINGA WAOMBA KUUNGWA MKONO

Innocent aka Lusso Mnyama  Isihaka aka Msangazi baharia WASHINDI wa mashindano ya kuimba singeli mkoa wa Iringa, Isihaka Msangazi ‘Baharia’ na Innocent Chanafi’ Lusso Mnyama’ wamewataka wadau kuwaunga mkono katika harakati zao kuupandisha muziki huo nyanda za Juu Kusini. Wakizungumza na SIMBAYABLOG jana mara baada ya kushinda mashindano ya kuimba sengeli katika mkoa wa Iringa yaliandaliwana kituo cha Radio cha Nuru Fm, Mshindi wa kwanza, Isihaka na Innocent walisema kuwa muziki huo unakuwa kwa kasi zaidi kutokana na ubora wake na kuonyesha uhalisia wa kitanzania zaidi. Walisema kuwa wawekezaji wakiwa wengi katika aina hiyo ya muziki ni lazima ajira iongezeke kupitia fani ya muziki hasa huu wa singeli ambao kwa sasa unazidi kuteka hisia za mashabiki wengi hasa katika sherehe mbalimbali. Kwa upande wake mshindi wa kwanza, Isihaka Msangazi alisema kuwa ushindi wake umekuja kutokana na kujituma kwa bidii katika mazoezi na kuupenda muziki huo am...