Na Friday Simbaya, Songea Hospitali ya Peramiho ya Mt. Josefu kwa kushirikiana na daktari bingwa wa macho Dr. Grasbon toka Ujerumani waliendesha kambi ndogo ya macho, ambapo ilianza tarehe 5-12/11/2012. Kambi hiyo ya macho ilifanikiwa kuona wagonjwa zaidi ya 120 toka sehemu mbalimbali ya Mkoa wa Ruvuma, ambapo wagonjwa 80 walipatikana na ugonjwa wa mtoto wa jicho (Cataract). Akizungumza na Gazeti la Mwenge hivi karibuni Dr. Wade Kabuka ambaye ni daktari wa macho katika Hospitali ya Peramiho, amesema tatizo la macho katika mkoa wa Ruvuma lipo na wagonjwa ni wengi. Amesema kuwa wakati wakiendesha kambi ya upimaji wa macho kwa ufadhili wa hospitali ya Peramiho kwa kushirikiana na Dr. Grasbon toka Ujerumani, wagonjwa waliojitokeza ni wengi sana, na wengi wao walikuwa na matatizo ya mtoto wa jicho. Amesema kuwa zaidi ya wagonjwa 120 walipimwa na kati yao 80 waligundulika na tatizo la mtoto wa jicho (Cataract), ambapo wote walipata matibabu kwa kuwekewa kioo ndani ya jicho. “Ugo...
Pamlomo-Sauti Ya Jamii (SYJ) is essentially a digital news platform that shares different types of news updates — social, political, economic, sports, entertainment, and community stories. From the context you’ve given, it is based in Iringa, Tanzania, and functions mainly as an online outlet (likely through social media such as Facebook, YouTube, or other channels) where audiences can get real-time updates.