Skip to main content

Posts

Showing posts from January 31, 2011

MTIHANI KIDATO CHA SITA: WASICHANA MAPOSENI KUWAONYESHA KAZI WAVULANA

  Sehemu ya wahitimu 53 wa Shule ya Sekondari ya Maposeni wa Kidato cha Sita wakiwa katika picha ya pamoja muda mfupi kabla ya kuanza sherehe ya Mahafali ya Pili 2011. Mkuu wa Shule ya Maposeni Sekondari, Humari Mapunda akisoma taarifa ya maendeleo ya shule kwa mgeni rasmi kwenye mahafali ya Pili ya kidato cha Sita 2011.   BAADA ya wasichana kung’ara Kidato cha Nne 2010, nao wasichana wa Kidato cha Sita katika Shule ya Sekondari ya Maposeni wamenena kuwaonyesha kazi wavulana katika mtihani ya Kidato cha Sita Mwaka 2011. Hivi karibuni Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) lilitangaza matokeo ya mtihani wa Kidato cha Nne uliyofanyika Oktoba mwaka jana yaliyoonyesha kuwa wasichana waliongoza kwa kiwango cha ufaulu. Hata hivyo, matokeo hayo yameonyesha kuwa kiwango cha ufaulu katika mtihani huo kimeshuka kwa asilimia 22 ikiliganishwa na matokeo ya mwaka 2009 kuwa wasichana walifanya vizuri zaidi kuliko wavulana, alisema Katibu Mtendaji wa NECTA, Dk Joyce Ndalichako. Wasi...