Skip to main content

Posts

Showing posts from August 31, 2016

MCHUNGAJI MPELI AMPONGEZA MAGUFULI KWA KUMJUA MUNGU

Mbeya:   Mkurugenzi na kiongozi wa taasisi ya dini ya Daily Bread Life Ministry Tanzania, Mchungaji James Mpeli Mwaisumbe amewasihi watanzania kumuombea Rais Dkt John Pombe Magufuli ili aweze kuliongoza taifa kwa haki, amani na upendo. Alisema kuwa ili Tanzania iweze kusonga mbele, waislamu, wakristo,viongozi wa siasa, serikali na watanzania kwa ujumla lazima waliombee taifa na viongozi wake kwa Mungu ili kuweza kudumisha amani na mshikamano viliyopo. Mchungaji Mpeli alisema hayo wakati wa sherehe ya kumuaga Mchungaji Raphael Mwasifiga wa Kanisa la Baptist, Kanani lililopo Sinde Makunguru, Mwanjelwa jijini Mbeya.  Mchungaji huyo mwalikwa alisema kuwa anavutiwa na kiongozi wa nchi kwa sababu ni mcha Mungu na katika maneo yake kumi anayozungumza hakosi kumtaja Mungu. Alisema kuwa taifa ni kitu cha muhimu kuliko vya vyama siasa na kuwaomba wakristo, waislamu viongozi wa siasa na serikali kuliombea taifa ili amani na mshikamano ambayo havipatikani Afrika i...