Skip to main content

Posts

Showing posts from December 15, 2016

MICHEZO YA TANO YA MAMLAKA YA USIMAMIZI WA BANDARI TANZANIA YATIMUA VUMBI TANGA

Tanga, MKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Deudence Kakoko, amewataka wafanyakazi wa mamlaka hiyo kufanya kazi kwa bidii ili kwenda kasi ya Serikali ya awamu ya Tano. Akifungua michezo ya Tano ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (INTERPORTS GAMES) viwanja vya shule ya Sekondari ya Popatlal Tanga jana, Kakoko, alisema kila mfanyakazi wa Mamlaka hiyo anapaswa kujua wajibu wake. Alisema kasi hiyo iende sambamba na uboreshaji wa utoaji huduma bandarini na kuwa kivutio kwa wageni ili kuweza kuitumia kwa kushusha shehena zao bandari za Tanzania. Michezo hiyo inashirikisha wafanyakazi wachezaji kutoka Tanga ambao ni wenyeji, Dar es Salaam,, Mtwara na Bandari za Ziwa.

MAMBO 8 YA KUZINGATIA PINDI UNAPOTAKA KUSAFIRI

Na Jumia Travel Tanzania HAKUNA jambo linalokera kama kugundua kuwa umesahau kitu fulani ambacho kilikuwa kina umuhimu mkubwa sana kwenye safari yako uliyokwishaianza. Hali kama hii huwa inawatokea watu wengi hivyo kupelekea kuchelewa au wakati mwingine kuachwa kabisa na usafiri. Kuepukana na usumbufu huu hasa ukizingatia asilimia kubwa ya watu wako kwenye pilikapilika za kusafiri kipindi hiki cha sikukuu na shamrashamra za mwaka mpya, Jumia Travel (www.travel.jumia.com) ingependa kukutahadharisha kuzingatia yafuatayo ili safari yako iwe ya raha mustarehe. Tafiti kuhusu mahali unapokwenda Ni muhimu kufahamu mahali unapokwenda hasa umbali wake, itakugharimu kiasi gani kufika, hali ya hewa, gharama za maisha pamoja na mila na utamaduni za watu wanaoishi huko. Kama unasafiri mkoa ambao haujawahi kufika hapo awali ni vizuri ukafanya tafiti au ukaulizia kutoka kwa marafiki, ndugu na jamaa ili usiende kupata tabu ukifika.  Tambua usafiri utakaokufiki...

BODI YA FILAMU NCHINI YAWATAKA WADAU KUFIKISHA MISWADA YA FILAMU KUKAGULIWA KABLA YA KUIGIZWA

Bi.Deograsia Ndunguru ambaye ni Kaimu Mkuu wa Idara ya Sanaa na Habari, Chuo Kikuu Dodoma UDOM, hii leo akiwasilisha mada kwenye mafunzo ya siku tatu kwa wanatasnia wa filamu na maigizo mkoani Mara, yaliyoanza jana ukumbi wa shule ya Sekondari Mara. Mafunzo hayo yameandaliwa na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kupitia Bodi ya Filamu nchini.  Mtendaji Mkuu Taasisi ya Sanaa Bagamoyo, Dkt.Herbert Makoye, hi leo akiwasilisha mada kwenye mafunzo ya siku tatu kwa wanatasnia wa filamu na maigizo mkoani Mara, yaliyoanza jana ukumbi wa shule ya Sekondari Mara.  Wanatasnia wa filamu na maigizo mkoani Mara wakifuatilia mada kutoka kwa Mtendaji Mkuu Taasisi ya Sanaa Bagamoyo, Dkt.Herbert Makoye.  Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu nchini, Bi.Joyce Fissoo (kushoto), akizungumza wakati wa mafunzo hayo. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa mafunzo hayo jan...

TIGO YAZINDUA DUKA LA 'TEAM LEADERS' DEVIS CORNER TANDIKA TEMEKE

Msimamizi wa Biashara wa Kampuni ya Simu Tigo Dar es Salaam na Zanzibar, Nderingo Materu (wa pili kushoto), akikata utepe kuashiria uzinduzi wa duka dogo la Tigo Tandika Devis Corner leo. Kutoka kulia ni Meneja Mauzo wa Tigo Wilaya ya Temeke, Fadhila Saidi, Mwendeshaji wa duka hilo, Khadija Matambo na kushoto ni Meneja Huduma kwa Wateja wa kampuni hiyo, Isack Shoo. Hawa ndio waendeshaji wa duka hilo. Kutoka kushoto ni Victor Juma, David Ngwale na kiongozi wao Khadija Matambo. Meneja wa Tigo Uendeshaji wa huduma za Wateja , Isaack Shoo akihojiwa na wanahabari. Picha ya pamoja. Picha ya pamoja baada ya uzinduzi wa duka hilo. Na Dotto Mwaibale KAMPUNI ya Tigo inayoongoza kwa maisha ya kidijitali Tanzania, leo imezindua rasmi mpangbo mdogo wa maduka ya huduma kwa wateja unaofahamika kama maduka ya Team Leaders ambayo yatatoa huduma za kampuni moja kwa moja kutoka maeneo wanayokaa wateja.  Kwa mujib...

WANANCHI KIJIJI CHA MATIGANJOLA WAMESEMA WAKIPATIWA UMEME MAJI...

Lucia Mlowe, mbunge viti maalumu (Chadema) mkoani Njombe akizungumza na wananchi wa kijiji cha Matiganjola katika Halmashauri ya Wilaya ya Njombe jana. (Picha na Friday Simbaya) ​ NJOMBE: WANANCHI wa Kijiji cha Matiganjola katika Halmashauri ya Wilaya ya Njombe, mkoani Njombe wameiomba serikali kuwapelekea umeme ambao utasaidia kuwapo kwa huduma mbalimbali kijijini hapo ikiwepo kupandisha maji ya kisima. Wananchi hao wamesema kuwa kuto kuwapo kwa umeme kijijini hapo hata huduma ya maji inakosekanana pamoja na kuwapo kwa Tanki Kubwa ambalo lilijengwa miaka zaidi ya 15 iliyopita na hakuna maji. Wananchi wanatoa ombi lao kwa serikali mbele ya mbunge wa Viti maalum mkoa wa Njombe, Lucia Mlowe ili kufikisha suala hilo serikalini kupitia Bungeni. Lazaro Mwinami, Samson Nyagawa na Agustino Mgaya, ni baadhi ya wakazi wa Kijiji cha Matiganjola waliosema kuwa nyumba zao zimepewa namba kwa muda mrefu kupitia shirika la umeme nchini (TANESCO), lakini hawajapata umeme ...

RUAHA WATER PROGRAM (RWP)-SWAUM EXIT WORKSHOP

WWF has implemented Sustainable Water Access, Use and Management Programme (SWAUM) which aimed at achieving sustainable water resources management in the Great Ruaha River Catchment area through application of Integrated Water Resources Management (lWRM) principles and approaches. The SWAUM has now come to an end this year 2016 after a successful implementation for consecutive five years.