Skip to main content

Posts

Showing posts from October 11, 2014

NEC: Hakuna kura ya maoni bila daftari jipya

Rais Jakaya Kikwete akipokea Katiba Inayopendekezwa kutoka kwa Aliyekuwa Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba, Samuel Sitta wakati wa hafla iliyofanyika kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma juzi. Katikati ni Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein. Picha na Edwin Mjwahuzi  Dar es Salaam. Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema haitaendesha uchaguzi wa aina yoyote, wala kuitisha kura ya maoni hadi kazi ya kuboresha daftari la kudumu la wapiga kura itakapokamilika.

Maofisa polisi 120 watimuliwa CCP

Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Ernest Mangu   Moshi . Maofisa wa Polisi wapatao 120 wa Jeshi la Polisi, waliokuwa wakihudhuria mafunzo ya kupandishwa vyeo katika Chuo cha Taaluma ya Polisi Moshi (MPA), wametimuliwa chuoni hapo.

KATIBU MKUU WA CCM AVUNA WANACHADEMA NYOLOLO

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Mbunge wa jimbo la Mufindi Kusini Mh. Menrad Kigola wakati alipowasili katika mashamba ya chai ya Ngwazi yanayomilikiwa na kampuni ya Uniliver wilayani Mufindi ambapo pia alishiriki kuchuma chai akishirikiana na Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa ,Ittikadi na Uenezi wakati wa ziara yake katika jimbo hilo, Kinana yuko katika ziara ya siku 30 ya mikoa ya Pwani, Tanga na Iringa akikagua Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 na kuhimiza wananchi kushiriki katika shughuli za maendeleo na uhai wa Chama cha Mapinduzi ambapo kesho anahitimisha ziara hiyo kwa kufanya mkutano mkubwa wa hadhara mjini Iringa. Katika mkutano uliofanyika kijiji cha Nyololo   aliyekuwa Katibu wa CHADEMA  Kijiji cha Igowole Bw. Josephat Sibadi Soda amerejea CCM  baada ya uongozi wa chama hicho kutomlipa madeni ya vifaa mbalimbali alivyochukua madukani wakati wa ujenzi wa mnara wa marehemu Daud Mwangosi aliyeuwawa wakat...