Skip to main content

Posts

Showing posts from November 27, 2015

MAPITIO YA MAGAZETI YA LEO IJUMAA JIONI

MEYA WA MANISPAA YA IRINGA KUJULIKANA DESEMBA 2

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Jimbo la Iringa mjini kimekanusha vikali kuwapo kwa mvutano katika mchakato wa kumpata meya atakayoongoza baraza la halmashauri ya manispaa ya Iringa kama ilivyoripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari. Wakizungumza na wanahabari jana mjini hapa Mwenyekiti wa wilaya ya Iringa mjini Frank Nyalusi na mjumbe wa mkutano mkuu wa chadema na mbunge wa jimbo la Iringa Mjini Mchungaji Peter Msigwa pamoja na madiwani wateule wa chama hicho, Nyalusi alisema kuwa habari iliyoandikwa na moja ya gazeti la kila siku la hapa nchini ni uzushi na wa kupuuzwa. Nyalusi amesema kuwa hawawezi kupuuza kila wanachoambiwa maana hakuna upuuzi ulio upuuzi mtupu hovyo waulizeni walipomtoa huyo meya wanayetuletea na kwanini ni huyo na siyo wale waliokuwa wakitajwa tajwa na ccm wasahau kabisa kumpata meya katika baraza la madiwani. Amesema kuwa uzushi huo umeendikwa kwa lengo la kuuza magazeti hivyo jamii inapaswa kusubiri jina ambalo litapitishwa na kamati ku...

Waziri Mkuu Mh Kassim Majaliwa afanya ziara ya kushtukiza Bandarini...!

  Waziri Mkuu Mh Kassim Majaliwa leo ameamuru kukamatwa kwa maafisa kadhaa wa Mamlaka ya Mapato (TRA) na wengine kufukuzwa kazi baada ya kufanya ziara ya kushtukiza Bandarini na kukuta uozo . Maafisa hao wametakiwa kusalimisha hati zao za kusafiria, nah ii imekuja baada ya kugundulika kuwa kuna makontena 349 yenye thamani ya zaidi ya bilioni 80 ambayo data za Mamlaka ya Bandari inazo lakini katika mtandao wa TRA hayaonekani.

BINAGI RADIO: KILICHOJIRI MAHAKAMA KUU KANDA YA MWANZA KUHUSU MWILI WA MAWAZO

Jana  Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza ilitengua zuio la Jeshi la Polisi Mkoani hapa la kuzuia ibada ya mazishi ya kuuaga mwili wa aliekuwa Mwenyekiti wa Chadema Mkoani Geita Alphonce Mawazo alieuawa kwa kukatwa mapanga na watu wasiojulikana Novemba 14 mwaka huu Mkoani humo.

MAKUNDI YA JAMII ASILIA YA WAHADZABE, WABARABAIG, WAMASAI WAIOMBA SERIKALI KUWATAMBUA KAMA JAMII NYINGINE!

Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu, Mh. Idd Ramadhan Mapuri (katikati) akizindua taarifa ya Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu kuhusu utafiti wa Hali ya Haki za watu wenye kuishi maisha asilia Tanzania. kushoto kwake ni Katibu Mtendaji wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Bi. Mary Massay na (kulia) ni mmoja wa wajumbe walioshiriki kuandaa ripoti hiyo, kutoka nchini Kenya katika taasisi ya ACHPR, Dk. Naomi Kipuri.(Picha zote na Andrew Chale, Modewjiblog ). Na Andrew Chale, Modewjiblog [DAR ES SALAAM-TANZANIA] Jamii ya watu wa asili na makundi yao wameiomba Serikali ya Tanzania kutambua uwepo wao hapa nchini ikiwemo kuwatangaza kwa mema na kuwasaidia kwa misingi ya haki, hutu na kimaendeleo kama watu wengine wanaotambulika ndani na nje ya mipaka yao. Hayo yameelezwa mapema leo jijini hapa wakati wa uzinduzi wa taarifa ya Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu kuhusu utafiti wa Hali ya Haki za watu wenye kuishi maisha asilia Tanzania wakiwemo makabila ya Wa...