Skip to main content

Posts

Showing posts from September 2, 2015

DK SLAA AMWAGA MANYANGA RASMI, AACHA SIMANZI UKAWA

DAR ES SALAAM:   Na Habib Shaban KATIBU mkuu wa CHADEMA Dkt Willbroad Slaa ameibuka na kusema aliamua kuachana na CHADEMA na siasa kwa ujumla tangu tarehe 28/08/2015 baada ya Mbunge wa Monduli Edward Lowasa kujiunga na CHADEMA, kwa kile alicho dai kuwa asingeweza kushiriki kumsafisha mtu mwenye madhambi na badala yake aliona ni vyema ajiengue kwakuwa yeye sio muumini wa siasa za ulaghai. Dkt Willbraod Slaa. Picha na Moshi Shaban Mallema Kauli hiyo ameitoa katika mkutano na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam, amabapo amesema ameamua kayasema hadharani kwa kile alicho dai kuna upotoshwaji unao endelea kuwa yuko likizo na kwamba atajiunga na shughuli za chama hicho mbele ya safari, huku akidai kuwa hakuwa likizo na wala hakupewa barua yoyote ya likizo. Hata hivyo amesema alijaribu mara kadhaa kuandika baraua za kujiuzuru lakini hakuweza kusikilizwa na mtu yoyote, na baadae aliamua kuchukua uamuzi wa kuchana shughuli za chama hicho, na kwamba uvumi ulioku...

MMLIKI WA ST. MATHEW ACHOMOLEWA KESI YA TALAKA NA MGAWANYO WA MALI

Na Mwandishi wetu MAHAKAMA ya Mwanzo Mbagala, Dar es Salaam imesema haiwezi kumuamuru Mmiliki wa nne za Shule za Sekondari, St Mathew na St Marks ,Thadei Mtembei kutoa talaka kwa Magreth Mwangu kutokana na ndoa yao kuwa batili. Akisoma hukumu hiyo leo, Hakimu Rajab Tamambele alisema ndoa aliyofunga Mwangu pamoja na Mtembei ambayo ni ya kimila ni batili kwa kuwa mdai hakutoa cheti cha ndoa hiyo ilipofungwa. Alisema kwa misingi hiyo, mahakama haiwezi kumuamuru Mtembei kutoa talaka kwani aliwasilisha cheti cha ndoa ya mke mmoja aliyoifunga mwaka 1985. pia alisema mahakama hiyo haiwezi kugawa mali kama ambavyo mdai ameiomba mahakama, ambapo amesisitiza kuwa mgawanyo wa mali unatokana na ndoa halali ambayo baba na mama wanaishi pamoja. ‘’Mashahidi wote wameeleza kuwa Mtembei na Mwangu walikuwa wanakutana hoteli ya Sleep Inn. Kwa hivyo mahakama inaona kuwa uhusiano kati ya mdai na mdaiwa ulikuwa wa kimapenzi pekee au hawara na kwa lugha ya kistaarabu tunaita mzazi...