Skip to main content

Posts

Showing posts from May 17, 2018

WALIMU MANISPAA YA IRINGA WAMCHARUKIA MKURUGENZI KUHUSU MADENI YAO

WALIMU wa Manispaa ya Iringa wameomba Mkurugenzi wa Halmashauriya Manispaa ya Iringa kuwalipa madeni walimu wote fedha zao za uhamisho wanazodai, ambaz.o wanadai kwa muda mrefu.  Akizungumza na waandishi wa habari jana ofisini kwake Katibu wa Chama cha Walimu (CWT) manispaa hiyo, Fotunatafatuma Njalale, alisema pamoja na serikali kusema kuwa haitaki kuzalisha madeni mapya ya walimu, bado kumekuwa na uhamisho wa walimu kwenda kwenye vituo vipya bila kulipwa fedha za uhamisho.  Njalale alisema kuwa wapo walimu waliohamishiwa nje ya Walaya ya Iringa na walikwenda kuripoti kwa nauli zao na baadaye kurudi kudai posho za usumbufu nauli na usafiri wa mizigo yao,  Alisema kuwa walimu hao wa Manispaa wanadai pesa ya usumbufu kutoka eneo moja kwenda nyingine, wakati wale walimu wa vijijini wanatakiwa kulipwa pesa ya usumbufu na kujikimu.  Alisema madai hayo ni ya muda mrefu lakini hawajalipwa hata senti huku wakilazimishwa kwenda kwenye vit...