Skip to main content

Posts

Showing posts from November 10, 2015

MFUMUKO WA BEI ZA BIDHAA MBALIMBALI WATIKISA SOKO KUU JIJINI MWANZA

Kwa takribani Wiki mbili sasa, Mfumuko wa bei za bidhaa mbalimbali kupanda katika Soko Kuu la Jijini Mwanza umeendelea kuwaliza watumiaji wa soko hilo. Na George Binagi-GB Pazzo Mfumuko huo unalalamikiwa na pande zote mbili kwa maana ya wauzaji na wanunuaji sokoni hapo, ambapo wameomba hatua za haraka kuchukuliwa ili kiweka mambo sawa. Bei kwa nafaka zote sokoni hapo zimepanda bei hadi shilingi 1,000 kwa kila moja tofauti na hapo awali ambapo bidhaa iliyokuwa ikiuzwa shilingi 15,000 sasa inauzwa kati ya 2,000 hadi 2,500 ambapo steki ya nyama imepanda bei kutoka shilingi 5,000 hadi shilingi 8,000 huku nyama mchanganyiko ikiuzwa shilingi 6,000 kutoka 4,000 za awali. Mwenyekiti wa Soko hilo Hamad Nchola amesema kuwa mfumuko huo umesababisha na mazao ya wakulima kupungua katika maghala yao kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo uhaba wa mavuno kutokana na ukosefu wa mvua katika msimu uliopita, pamoja na wafanyabiashara kutoingiza sokoni bidhaa katika kipindi cha ucha...

MAGAZETI LEO JUMATANO